• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Bahi Mmenifurahisha: Jafo

Imechapishwa: May 8th, 2019

Benton Nollo, Bahi

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani S. Jafo (Mb) ameupongeza Uongozi wa Wilaya ya Bahi kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za Afya unaoendelea katika Halmashauri hiyo.

Akizungumza katika ziara yake ya kikazi wilayani hapa Jafo ameonyesha kuridhishwa kwake na wakati anapokea taarifa ya Wilaya ya Bahi kuhusu maendeleo ya ujenzi wa miradi ya Afya na kisha kutembelea ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambayo ipo katika hatua ya lenta.

“Hakika Bahi mmefanya kazi nzuri  mmejenga kwa kasi ya ajabu huku ubora ukizangatiwa katika majengo yote na  bado mmesimamia matumizi mazuri ya fedha za mradi kwa kuwapa vibarua  kazi hii ya ujenzi". Alisema Jafo na kuongeza.

"Niseme wazi kuwa Bahi mmenifurahisha kwa sababu mmeweza kutafsiri vizuri mfumo wa ujenzi pasipo kutumia Mkandarasi yaani “Force Account” ambao unatumia fedha kidogo na mmeweza kutumia nguvu kazi mliyonayo ya vijana wa mgambo kufyatua matofali na vibarua ambao ni vijana kutoka hapa hapa Bahi kujenga majengo ya Afya hongereni sana kwa hili” Alisema Jafo.

Pamoja na kuwapongeza viongozi hao pia aliwataka kumaliza tofauti zilizopo kati ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo na Mbunge kwa kuwasisitiza kila mmojawao kutekeleza majukumu yake pasipo kuingiliana wala kukwamishana.

“Lengo letu sote ni kuleta maendeleo kwa Wananchi kwa hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri tekeleza majukumu yako pasipo kumuingilia Mbunge na Mbunge naye aendelee kutekeleza majukumu yake ya Kibunge tena anafanya vizuri sana na miradi yote hii mnayopata ni jitihada zake Bungeni kwa hiyo msimkwamishe mpeni ushirikiano wa kutosha” Alisema Jafo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Belinith Mahenge amemueleza Waziri Jafo kuwa Wilaya ya Bahi ni moja kati ya Wilaya za Dodoma zinazofanya vizuri katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Mwanahamisi Munkunda amesema kuwa ujenzi wa vituo vitatu vya Afya umeshakamilika na vitafunguliwa hivi karibuni wakati Hospitali ya Wilaya ikiwa katika hatua ya lenta.

“Pamoja na changamoto chache ambazo tunakutana nazo katika utekelezaji wa miradi hii kama vile ushiriki mdogo wa wananchi katika kuchangia nguvu kazi, kukosekana kwa Mhandishi wa Halmashauri lakini tumeweza kukabiliana nazo na kuhakikisha hazikwamishi ujenzi wa miradi yetu ya Afya” Alisema Munkunda.

Ujenzi wa Hospitali za Wilaya unaondelea kote nchini na unatarajiwa kukamilika Juni 30, 2019.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani S. Jafo (Mb), akiwasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bahi tarehe 08 Mei, 2019.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani S. Jafo (Mb), akiongea na viongozi pamoja na wataalam mbalimbali waliojitokeza wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bahi tarehe 08 Mei, 2019.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani S. Jafo (Mb), akiiendelea na ukaguzi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bahi tarehe 08 Mei, 2019.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Selemani S. Jafo (Mb), akiangalia matofali maalum kwa ajili ya ujenzi wa jengo la mionzi ambayo yamefyatuliwa na vijana wa Jeshi la Akiba ambao wamepewa kazi hiyo kwa lengo la kurahisisha kazi ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bahi wakati wa ziara yake tarehe 08 Mei, 2019.

Muonekano wa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD) ambalo ni miongoni mwa majengo saba yanayoendelea kujengwa katika Hospitali ya Wialaya ya Bahi.

Muonekano wa Jengo la Utawala ambalo ni miongoni mwa majengo saba yanayoendelea kujengwa katika Hospitali ya Wialaya ya Bahi. 

(Picha zote na Benton Nollo).

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa