MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MAAFISA ELIMU KATA PAMOJA NA WALIMU WAKUU YAFANYIKA WILAYANI BAHI.
Kupitia Mpango wa Shule bora leo tarehe 10/02/2025 yamefanyika Mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa Shule.
Mafunzo haya yana lengo la kuongeza ushirikiano baina ya Walimu Wakuu,Maafisa Elimu Kata na watumishi walio chini yao ili kuboresha utendaji kazi na kufanikisha dhana nzima ufundishaji na ujifunzaji ili kupata matokeo bora.
Mafunzo hayo yamefunguliwa na Afisa Elimu Wilaya Ndg.Boniface Wilson na yatafanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kuanzia leo na kutamatika siku juma tano tarehe 13/02/2025.
Aidha,mafunzo haya yatakua endelevu kwa kuanzisha jumuiya za ujifunzaji ngazi ya Shule lengo kuu ikiwa ni kuzidi kupeana uzoefu katika usimamizi wa shule.
Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
Anuani: S.L.P 2993 DODOMA
Simu: +255 762077589
Simu: +255 762077589
Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz
Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa