• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Munkunda Akabidhi Vifaa vya Milioni 10.8

Imechapishwa: December 1st, 2020

Na Benton Nollo na Bernard Magawa DMC, Makanda

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amekabidhi Kompyuta tano pamoja na mashine moja ya kuchapisha (printa) zenye thamani ya shilingi milioni 10.8 katika Shule ya Sekondari CHONAMA iliyopo Kata ya Makanda wilayani Bahi mkoani Dodoma.

Munkunda amekabidhi vifaa hivyo wakati akiwa kwenye ziara yake ya siku moja katika kata hiyo na kufika shuleni hapo kukagua shughuli za maendeleo ya kitaaluma tarehe 01 Desemba 2020.

Amesema ameamua kutoa vifaa hivyo kwa Shule ya Sekondari CHONAMA kama motisha kutokana na shule hiyo kufanya vizuri kitaaluma katika Wilaya ya Bahi na kwamba kwa kufanya hivyo itawarahisishia Walimu katika shughuli zao za ufundishaji na kuongeza ufaulu zaidi kwa wanafunzi.

“Nimewaletea kompyuta tano na printa moja kama motisha kwa shule yenu  kwa kuwa mmekuwa mkifanya vizuri katika mitihani ya Kidato cha Nne Kiwilaya.” Amesema Munkunda na kuongeza kuwa:

“Naamini vifaa hivi vitawasaidia katika kuchapisha mitihani mbalimbali ikiwemo ile ya kuwapima watoto walau kila wiki”.

Pamoja na kuwapongeza walimu wa shule hiyo kwa juhudi zao, Munkunda amesema bado haridhishwi na kiwango cha ufaulu wanachokipata ukilinganisha na idadi ndogo ya wanafunzi waliopo shuleni hapo hivyo aliwaagiza waalimu hao kuongeza  bidii  ili waweze kufaulu  zaidi kuliko sasa.

“Kulingana na idadi ndogo ya wanafunzi mlionao bado mnayo nafasi ya kufaulisha zaidi hivyo, ongezeni  juhudi  ikibidi hata  kutumia ‘table teaching’ ili muwe na ufanisi zaidi katika matokeo yenu.” Amesema Munkunda.

Akizungumza baada ya kupokea vifaa hivyo Mkuu wa Shule Msaidizi wa Shule ya Sekondari CHONAMA, Titus Yosea amemshukuru kiongozi huyoa kwa kuthamini mchango wao kitaaluma na kuahidi kuwa vifaa hivyo vitatumika ipasavyo ili kuinua zaidi kiwango cha taaluma shuleni hapo  na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kwa niaba ya Walimu wenzangu na Manafunzi wa Shule ya Sekondari CHONAMA nakushukuru sana kwa kutuletea vifaa hivi, nasi tutavitumia kwa maandalizi mbalimbali ya masomo na mitihani ya mara kwa mara hivyo tunaamini kwa kufanya hivyo kiwango cha ufaulu katika shule yetu kitaongezeka.” Amesema Mwalimu Yosea.

 Shule ya Sekondari CHONAMA ni mwiongoni mwa shule za sekondari 21 wilayani Bahi na imekuwa ndiyo shule pekee inayofanya vizuri katika matokeo ya Kidato cha Nne katika wilaya na Mkoa wa Dodoma.


Matukio katika Picha:

Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda wakati akikabidhi vifaa hivyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa