• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Afya

Wilaya ina vituo 43 vya kutolea huduma za afya, vikiwemo Vituo vya Afya 6 na Zahanati 37, kati ya zahanati hizi 2 zinamilikiwa na mashirika ya dini.  Wilaya inaendelea na ujenzi wa zahanati 2 katika vijiji vya Chonde na Mayamaya. Pia, Wilaya inapanua Kituo cha Afya Bahi ili kuweza kutoa huduma za upasuaji wa dharura.  Huduma za afya zinatolewa kwa kuzingatia maeneo muhimu ya afya ya Uzazi na Mtoto, Afya ya Kinga (Udhibiti na Kinga ya Magonjwa kwa Jamii), Udhibiti wa magonjwa ya eneo husika (maalum) kama vikope na kichocho. Uimarishaji wa huduma za kiutawala, miundombinu, vifaa na dawa (tiba). Wilaya imefanikiwa kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi kutoka 9 mwaka 2000 hadi kufikia vifo 4 mwaka 2016. Pia, katika kipindi hiki, Wilaya imefanikiwa kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka mitano kutoka vifo 40 hadi kufikia vifo 12 mwaka 2016.

Aidha, sekta ya afya bado ina upungufu mkubwa wa watumishi kulingana na ikama.  Hadi sasa kuna jumla ya watumishi 369 kati ya 779 wanaohitajika na hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 410.

Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Wilaya inaupa kipaumbele ili kuboresha afya za wakazi wake na ilijiwekea lengo la kusajili kaya 15,269 (31%) kati ya kaya 49,554 za Wilaya kwa miaka mitatu (2015 hadi 2017) chini ya mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS). Katika kipindi hicho Wilaya imefanikiwa kusajili kaya 8,190 (54%) ya lengo, ambapo shilingi 184,270,000.00 zimekusanywa. Umuhimu wa kujiunga na mfuko huu bado utaendelea kuwa ajenda ya kudumu katika vikao vya Kiserikali, vituo vya Afya na Zahanati.

Elimu ya mapambano dhidi ya UKIMWI inatolewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikisisitiza njia mbalimbali za ueneaji, jinsi ya kujikinga pamoja na umuhimu wa mabadiliko ya tabia kwa jamii hasa vijana ambao ndio waathirika wakubwa katika jamii yetu. Kampeni dhidi ya UKIMWI inaendeshwa kwa kutoa elimu na upimaji wa VVU wakati wa matukio ya sikukuu za kitaifa na kimataifa ikijumuisha  sikukuu ya wakulima, siku ya UKIMWI duniani.

Makundi maalum yanashirikishwa katika kampeni, ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa baa, wakunga wa jadi, viongozi wa dini, kisiasa na wasanii (vikundi vya ngoma). Wazazi hupatiwa elimu siku za kliniki ya mama na mtoto. Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali ni wadau muhimu katika kutoa elimu na huduma dhidi ya UKIMWI. Viongozi wa dini wanatoa elimu kwa waumini, pamoja na viongozi wa kisiasa na jamii yote kupitia mikutano ya hadhara.

Wananchi waliopima kwa hiari kati ya Januari hadi Desemba, 2015 ni 15,435 (Me 5,893 na Ke 9,542). Waliogundulika kuwa na maambukizi ya VVU ni 377 (Me 143, Ke 234) sawa na 2.4%. Wilaya ina vituo 5 vinavyotoa huduma ya dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV’s), ambapo wagonjwa 1,420 wanahudumiwa kati ya wagonjwa 2,000 walioandikishwa. Vituo hivyo ni Babayu, Bahi, Chipanga, Mtitaa na Mundemu.  Mpango wa kuongeza vituo vingine unaendelea, huduma mseto za Kifua Kikuu na UKIMWI zimeanzishwa na kuimarishwa ambapo kati ya wagonjwa 91 wa Kifua Kikuu 11 wamegundulika kuwa na maambukizi ya VVU katika kipindi hicho.

Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI. July 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE. JOACHIM THOBIAS NYINGO AFANYA KIKAO CHA KUJADILI MIKAKATI MBALIMBALI YA MAENDELEO KUELEKEA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 KWA IDARA MBALIMBALI NA VITENGO BAADA YA KUPOKEA BILIONI 1.7.

    July 04, 2025
  • MKURUGENZI WA MRADI WA "TUINUKE PAMOJA" CHINI AGHAKAN FOUNDATION WAKISHIRIKIANA NA TGNP ATAMBULISHA MRADI HUO KATIKA MANEJINENTI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI.

    July 03, 2025
  • UHAMISHO NA UTEUZI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI

    July 23, 2025
  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa