• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kilimo na Umwagiliaji

Malengo ya Kilimo:

Katika msimu wa mwaka 2015/2016, Wilaya ilijiwekea malengo ya kulima hekta 167,870 kati ya hizo hekta 114,940 ni mazao ya chakula na hekta 52,870 mazao ya biashara. Aidha, kiuhalisia jumla ya Hekta 147,320 zilitumika kulima mazao ya chakula na biashara.

Matarajio ya mavuno yalikuwa Tani 139,122 za mazao ya chakula na Tani 57,780 za mazao ya biashara. Kwa mazao ya chakula ambayo ni (Mtama, Uwele, Mpunga, Muhogo mbichi, Kunde, Njugu mawe na Viazi vitamu) uzalishaji halisi zilitarajiwa kupatikana Tani 75,465.66. Mahitaji ya chakula kwa mwaka kwa wakazi wa Wilaya ya Bahi ni Tani 68,360.9. Hivyo Wilaya ingefanikiwa kuzalisha ziada ya Tani 7,104.76 za mazao ya chakula. Kwa mazao ya biashara ambayo ni (Ufuta, Alizeti na Karanga) uzalishaji halisi ni Tani 32,528.10.

Hata hivyo, katika mwaka wa 2015/2016 Wilaya ilivamiwa na ndege waharibifu wa mazao (Kwelea Kwelea) na kusababisha athari katika vijiji 25 kati ya 59. Tathimini iliyofanywa na kamati ya maafa ya Wilaya ilionesha Ekari 19,121.3 za mazao ya chakula ziliharibiwa vibaya. Wilaya kwa kushirikiana na kitengo cha udhibiti wadudu waharibifu kanda ya Kati iliweza kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na ndege hao. Pia Wilaya imewasilisha maombi maalumu ya mbegu za mazao ya Mtama, Mihogo na Viazi lishe katika kitengo cha maafa katika ofisi ya Waziri Mkuu ili kusaidiwa, wananchi waweze kupata mbegu kwa ajili ya msimu wa 2016/2017. Wilaya imefanikiwa kupata mbegu jumla ya kilo 4,135 za mtama aina ya macia na kilo 1000 za mpunga (Saro – 5) na zoezi la kuzisambaza katika vijiji husika limekamilika.

Kwa msimu wa mwaka huu 2016/2017 Wilaya imejiwekea malengo ya kulima hekta 157,226 na kuvuna Tani 249,299 za mazao ya chakula, Tani 72,000 mazao ya biashara na Tani 8,442 za mazao ya mbogamboga na matunda.

Wilaya imepokea fedha za mradi kutoka JICA Shilingi 413,000,000.00 ambazo zimetumika katika shughuli za ukarabati wa eneo la chanzo cha maji kwa ajili ya skimu za Mtazamo/Uhelela na kazi hiyo inatarajiwa kukamilika tarehe 15/01/2017.

Aidha, katika msimu huu wa kilimo hali ya unyeshaji mvua imekuwa chini ya wastani kama inavyoonekana kwenye jedwali lifuatalo:-

 Jedwali 1: Hali ya unyeshaji mvua katika wilaya ya Bahi kwa miezi 2.

Mwezi

Kiasi (mm)

Siku

Desemba

48.6

3

Januari

33.9

2

Jumla

82.5

5

 

Sekta ya Ushirika:

Wilaya ina jumla ya vyama vya ushirika 25. Kati ya vyama hivyo, vyama vya Akiba na Mikopo ni 18 na Vyama vya Mazao ni 8 vikiwa na jumla ya wanachama 3,307 (wanaume 1,934 na wanawake 1,373).  Lengo kuu la vyama hivi ni kuinua hali ya maisha ya wanachama kwa kuhamasisha wananchi kuweka akiba na kupata mikopo ya fedha kwa ajili ya kufanyia biashara na kununua pembejeo za Kilimo ili kuongeza uzalishaji.

Vyama vya Akiba na Mikopo vimeongezeka kutoka 6 mwaka 2010 hadi 18 mwaka 2015/2016, Vyama vya mazao (AMCOS)  kutoka 0 mpaka 7na vikundi 17 hadi 47 pamoja na wanachama kutoka 982 hadi kufikia 3,307.

Vilevile Hisa, Akiba na Amana za wanachama zimeongezeka; Idadi ya hisa za wanachama zimeongezeka kutoka shilingi 10,939,000.00 mwaka 2010 na kufikia shilingi 55,534,000.00 mwaka 2015/2016. Akiba za wanachama zimeongezeka kutoka shilingi 22,419,300.00 hadi kufikia 84,653,000.00 na amana za wanachama kwa sasa zipo shilingi 15,752,000.00. Jumla ya mikopo yenye thamani ya shilingi 276,643,642.00 imetolewa kwa wanachama wa SACCOS.

Pia, wanachama 102 wa AMCOS wamejiandikisha katika mfuko wa Jamii wa NSSF kwa ajili ya kupata mafao ya uzeeni na kupatiwa huduma za matibabu na mazishi.

 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa