• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kipanga: Ujenzi Vyuo vya VETA Nchini Mwisho Machi 2021

Imechapishwa: January 20th, 2021

Na Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omary Kipanga (Mb) ameagiza ujenzi wa vyuo vyote vya VETA unaoendelea nchi nzima kukamilika kabla ya tarehe 31 Machi 2021 ili majengo hayo yaanze kutumika mwaka huu.

Kipanga ametoa agizo hilo tarehe 20 Januari 2021 alipotembelea na kukagua ujenzi wa chuo cha VETA Wilaya ya Bahi ambapo hakuridhishwa na kasi ya ujenzi wa chuo hicho ambao unasimamiwa na Uongozi wa Chuo hicho kwa kutumia Force Account kwa gharama ya shilingi bilioni 1.6.

“Binafsi niseme wazi sijaridhishwa kabisa na mwenendo wa ujenzi wa chuo hiki na namna mlivyoandaa mpangilio wa kazi zenu, nitarudi tena hapa baada ya wiki moja na nitakapo kuja nikute kila jengo lina fundi wake na wanafanya kazi vinginevyo tusilaumiane kwani siwezi kuacha uzembe huu uendelee.” Amesema Kipanga na kuongeza;

“Niagize wale wote wanaosimamia miradi ya ujenzi wa vyuo vya VETA nchini kuhakikisha wanakamilisha miradi hii kabla ya tarehe 31 Machi 2021, na viongozi wa maeneo hayo simamieni kikamilifu ujenzi huo ili majengo hayo yaweze kufunguliwa na kuanza kazi mapema mwaka huu.”

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri huyo, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda ameahidi kusimamia kwa ukaribu na kuhakikisha ujenzi huo unakamilika haraka iwezekanavyo.

“Ujenzi umekuwa wa kusuasua sana, hata mimi sifurahishwi wala siridhishwi na ujenzi wa chuo chetu cha VETA Bahi, tuna watoto wengi mitaani ambao hawakufaulu kuendelea na masomo mengine na hatuna pa kuwapeleka zaidi ya VETA, sielewi tatizo liko wapi labda kwa sababu mamlaka haipo Halmashauri ipo wizarani.” Amesema Munkunda na kuongeza;

“Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kweli hili linatuchafua sisi kama Wilaya kwa sababu mambo haya hatujazoea, sisi tumekuwa tukifanya vizuri katika miradi mingine ambayo fedha zilipita Halmashauri.”

Naye, Makamu Mkuu wa Chuo cha VETA Mkoa wa Dodoma, Stanslaus Ntibala amesema kusuasua kwa ujenzi huo kunatokana na changamoto mbalimbali ikiwemo vifaa vya ujenzi kuchelewa kupelekwa na wazabuni ilhali tayari walishalipwa.

 Ujenzi wa chuo cha VETA Bahi unaojumuisha ujenzi wa majengo 17 ulianza mwezi Mei 2020 na ulitakiwa kukamilika mwezi Desemba 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa