• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Munkunda: Mauaji ya Mgaya ni Ukatili Mkubwa

Imechapishwa: April 8th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amesema mauaji ya Mwalimu Heladius Lucas Mgaya, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chilingulu aliyeuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana usiku tarehe 06 Aprili 2020 ni ukatili mkubwa ambao hautakiwi kufimbiwa macho.

Munkunda ameyasema hayo wakati wa ibada fupi ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Mgaya iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi tarehe 08 Aprili 2020.

Mkuu huyo wa Wilaya amewahakikishia ndugu wa Marehemu kuwa Mwalimu Mgaya alikuwa ni mtu mwema sana. Aidha, amesema tukio lililotokea ni ukatili kama ulivyo ukatili mwingine na kamwe haukubariki ambapo amewaomba kutambua kuwa Serikali ipo kazini na wahusika watachukuliwa hatua stahiki kwani kazi hiyo tayari imeshaanza.

“Mimi na Mkurugenzi baada ya kupata taarifa za tukio hili mara moja tulikwenda eneo la tukio ambapo tuliungana na viongozi ngazi ya kata na kiukweli tunakemea matukio maovu kama haya na ninaahidi kuwa wale wote waliohusika vyombo vya dola vinaendelea na kazi na sharia itachukua mkondo wake”. Anasema Munkunda na kuongeza;

“Msione kwamba mlituletea kijana wenu Mgaya kwa kumsomesha kwa gharama kubwa amekuja kututumikia sisi Wanabahi ndo tunawapa zawadi ya kumrudisha akiwa kwenye sanduku, hapana, hapana kabisa na sisi tutaendelea kupambana kama Serikali kuhakikisha kwamba hili lililompata mtumishi mwenzetu, sumu hii iwe mwisho kwa sababu inawezekana tusipoikomesha itaendelea kututafuna sisi wote, maana yake sisi wote ni watumishi wa serikali bila kujali wewe unatumika katika eneo gani”.

Munkunda amewatoa hofu na kuwasihi watumishi katika wilaya hiyo kuwa watulivu na wavumilivu katika kipindi hiki kigumu ambapo Serikali inaendelea kulifanyia kazi suala hilo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga amewasihi watumishi wasiogope ijapokuwa tukio lililompata mtumishi huyo linasikitisha na linasononesha sana kwani ni ukatili mkubwa aliofanyiwa mtumishi huyo.

“Tukio hili ukilitafakali kibinadamu mioyo yetu inaguswa sana na unaona kabisa kutokea kwake ni kukosekana kwa upendo na wahusika kutokuwa na hofu ya mungu…sisi kama serikali wajibu wetu ni kufuatilia watoto wote kwenda shule sasa hili kwa ndugu zetu wa Chilungulu wakati Mwalimu Mgaya akitekeleza hilo alionekana kuwa kero kwao”. Amesema Dkt. Mganga

Kadhalika, Dkt. Mganga amewaomba viongozi wa dini kubuni mbinu mpya ya kuokoa roho za watu zilizopotea kwani maumivu yanayosababishwa na watu wasio na hofu ya mungu ni makali sana.

“…Penye upendo hatutegemei kukuta kitu kama hiki, hii ni chuki ndiyo maana imesababisha tukio kama hili ambalo linasononesha sana”. Amesema Dkt. Mganga.

 Mwalimu Heladius Lucas Mgaya alizaliwa tarehe 03 Septemba 1979 katika Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe. Aidha, aliajiriwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bahi mwaka 2004 na mpaka anafariki alikuwa ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Chilungulu, Kijiji cha Chilungulu Kata ya Mundemu wilayani Bahi.

PICHA NA MATUKIO:

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga akizungumza baada ya ibada fupi iliyofanyika kumuombea Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu. Ibada hiyo ilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza baada ya ibada fupi iliyofanyika kumuombea Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu. Ibada hiyo ilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  ya wilaya hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Bahi, Mohamed Msongo akisoma wasifu wa Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu. Wasifu huo umesomwa baada ya ibada ya kumuombea Marehemu ilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Katekista Henry Nchingu wa Kanisa Katoliki Bahi akiendesha ibada ya kumuombea Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu. Ibada hiyo ilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  ya wilaya hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Viongozi mbalimbali wakitoa salamu za pole kwa wafiwa na waombolezaji waliofika kutoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu. Salamu hizo zilitolewa baada ya ibada ya kumuombea Marehemu iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  ya Wilaya ya Bahi tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Bahi na waombolezaji wakitoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu Kata ya Mundemu. Heshima hizo zimetolewa baada ya ibada ya kumuombea Marehemu iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Ndugu na Mtoto wa Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu, Kata ya Mundemu wakilia kwa uchungu wakati wakitoa heshima zao za mwisho kwa mpendwa wao baada ya ibada  fupi ya kumuombea Marehemu iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Baba Mlezi wa Marehemu, Mwalimu Albert Yosef Mlowe akitoa shukrani kwa niaba ya Familia kwa viongozi wa Wilaya ya Bahi na waombolezaji waliojitokeza kutoa heshima zao za mwisho kwa Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu, Kata ya Mundemu baada ya ibada ya kumuombea Marehemu iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  hiyo tarehe 08 Aprili 2020 kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Kijiji cha Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi.

Baadhi ya Walimu wakitoa jeneza lenye mwili wa Marehemu Mwalimu Heladius Mgaya aliyeuawa na watu wasiojulikana wakati akirudi nyumbani kwake usiku tarehe 06 Aprili 2020 katika Kijiji cha Chilungulu, Kata ya Mundemu na kuupakia kwenye gari tayari kwa safari ya kuelekea kijijini kwao Iwungilo, Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe kwa ajili ya mazishi . (Picha zote na Benton Nollo).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa