• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mapogo: Tuwaonee Huruma Wajukuu Wetu

Imechapishwa: December 24th, 2019

Na Benton Nollo, Bahi

Wananchi wilayani Bahi wametakiwa kupanda miti na kutunza mazingira kwa faida ya sasa na vizazi vijavyo.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Bahi, Jeremia Mapogo wakati akizindua Kampeni ya Upandaji Miti wilayani humo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo tarehe 24 Desemba 2019, zoezi ambalo limefanyika katika Kijiji cha Bahi Sokoni.

Mapogo amesema kuwa miti ni rasilimali muhimu sana kwa mustakabali wa uhai wa binadamu na viumbe vingine duniani, hivyo inatakiwa kulindwa na kuhifadhiwa.

Amesema kuwa hali ya hewa ya Bahi imekuwa na ukame mkubwa kwa sababu kasi ya watu kuharibu mazingira kwa kukata miti ovyo ni kubwa mno.

“Ndugu zangu wananchi, mtakubaliana na mimi kuwa tumekuwa wabinafsi sana kwa kujijali sisi tuliopo duniani leo, tunakata miti ovyo ili kukidhi mahitaji yetu ya sasa bila kupanda miti mingine ya kutosha ili pia kizazi kijacho kije kunufaika nayo”. Amesema Mapogo na kuongeza.

“Hebu tujiulize leo, hivi babu na bibi zetu wasinge tunza mazingira, si tungekuwa kwenye jangwa la hatari. Basi kama ndivyo, tutambue kuwa tunawajibu mkubwa wa kutunza miti ya asili iliyopo na kupanda mingine mipya”.

Mapogo ametoa wito kwa wafugaji wanaoachia mifugo yao kiholela na kuchungisha miti ambayo inanunuliwa na kutunzwa kwa gharama kubwa na kutoa onyo kwamba yeyote atakayebainika kufanya hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha, akizungumza awali Afisa Mazingira Wilaya ya Bahi, Agnetha Maseko amesema kuwa lengo la wilaya hiyo kwa mwaka 2019/2020 ni kupanda miti milioni 1.5 lakini mpaka sasa Wakala wa Huduma ya Misitu Tanzania (TFS) imeipatia wilaya hiyo miche ya miti elfu 50.

 Maseko amesema tayari imeshagawanywa katika Kata 22 za wilaya hiyo na kila kata imepata miche 2,272.


Picha na Matukio:

Katibu Tawala Wilaya ya Bahi, Jeremia Mapogo akizungumza na wananchi waliojitokeza kushiriki uzinduzi wa Kampeni ya Upandaji Miti wilayani humo kwa mwaka 2019/2020 uliofanyika katika Kijiji cha Bahi Sokoni tarehe 24 Desemba 2019. Mapogo alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo.


Afisa Mazingira Wilaya ya Bahi, Agnetha Maseko akitoa taarifa ya utunzaji wa Mazingira wilayani humo kwa mgeni rasmi na wananchi waliojitokeza kushiriki uzinduzi wa Kampeni ya Upandaji Miti wilayani humo kwa mwaka 2019/2020 uliofanyika katika Kijiji cha Bahi Sokoni tarehe 24 Desemba 2019. 

Baadhi ya Wataamu na wananchi wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani) baada ya kushiriki uzinduzi wa Kampeni ya Upandaji Miti wilayani humo kwa mwaka 2019/2020 uliofanyika katika Kijiji cha Bahi Sokoni tarehe 24 Desemba 2019. (Picha zote na Benton Nollo)


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa