• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

462 Waishio Mazingira Magumu Kusomeshwa Bahi

Imechapishwa: February 8th, 2019

Benton Nollo, Bahi

Mfuko wa Elimu Wilaya ya Bahi umepitisha majina ya wanafunzi 462 wanaoishi katika mazingira magumu wilayani humo ili waweze kugharamiwa sare, viatu na madaftari baada ya kuwa wamefaulu kujiunga na masomo ya Kidato cha Kwanza mwaka 2019 katika shule mbalimbali.

Majina hayo yamepitishwa kwenye kikao cha Kawaida cha Mfuko huo kilichoketi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi tarehe 08 Februari, 2019 ambapo mwanafunzi mmoja kati ya hao anasoma Kidato cha Tatu katika Shule ya Sekondari Mundemu kwa kuwa mama yake anatatizo la kuongea (bubu) ambaye aliomba mtoto wake asaidiwe na mfuko huo.

Mfuko huo, umeidhinisha shilingi milioni 32.7 kati ya shilingi milioni 56 zilizopo katika mfuko huo zitumike kwa ajili ya kuwanunulia sare, viatu na madaftari. Aidha, wanafunzi watano wanaokwenda Shule ya Sekondari Mundemu wao pamoja na vifaa hivyo pia, watanunuliwa godoro moja kwa kila mmoja hivyo fedha zitakazotumika kwa ajili ya shughuli hiyo ni shilingi milioni 22.7 na shilingi milioni 10 zitatumika kwa ajili ya uhamasishaji na ufuatiliaji kwa kipindi cha mwaka mzima wa 2019.

Awali akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Mfuko huo, Mhe. Donald Mejiti alitoa angalizo na kusisitiza kuwa manunuzi yote ya vifaa vilivyoidhinishwa na wajumbe kwa ajili ya wanafunzi hao, yafuate utaratibu wa manunuzi ya umma na isitolewe fedha taslimu kwa namna yoyote ile bali zipelekwe shuleni kwa idadi ya wanafunzi husika na wataalam walisimamie suala hiyo kikamilifu.

Kwa Upande wake Afisa Elimu Wilaya ya Bahi, Upendo Lweyemamu ambaye ndiye Katibu wa Mfuko huo aliwaeleza wajumbe kuwa majina hayo yaliwasilishwa na Waratibu Elimu Kata kutoka kwenye Kata zote 22 za Wilaya ya Bahi wakishirikiana na Walimu Wakuu katika maeneo husika na anaamini kuwa viongozi katika maeneo hayo wamehusika kuidhinisha upatikanaji wake. 

Mfuko wa Elimu Wilaya ya Bahi ulianzishwa rasmi mwaka 2014 kwa lengo la kuwasaidia watoto wanaofaulu vema masomo yao lakini wazazi au walezi wao hawana uwezo wa kumudu gharama za kuwasomesha.

Kupata majina ya Wanafunzi hao bonyeza maandishi yenye rangi ya blue hapo chini:-

http://www.bahidc.go.tz/storage/app/media/uploaded-files/orodha-ya-wanafunzi-waliochaguliwa-kujiunga-na-kidato-cha-kwanza-2019-na-kusomeshwa-na-mfuko-wa-elimu-wa-wilaya-ya-bahi-1.pdf


Habari Katika Picha:

Mwenyekiti wa Mfuko wa Elimu Wilaya ya Bahi, Mhe. Donald Mejiti (wa kwanza kulia) akiongoza kikao cha kawaida cha mfuko huo kilichoketi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi  tarehe 08 Februari, 2019 na kupitisha majina 462 ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wamefaulu kujiunga na masomo ya Kidato cha Kwanza katika shule mbalimbali za Wilaya ya Bahi kwa mwaka 2019. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mhe. Mwanahamisi Munkunda na wa kwanza kushoto ni Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Bahi na Katibu wa Mfuko huo, Upendo Lweyemamu.


Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Bahi ambaye pia ni Katibu wa Mfuko wa Elimu Wilayani humo, Upendo Lweyemamu akiongea wakati wa kikao hicho. 


Mjumbe wa Mfuko wa Elimu Wilaya ya Bahi ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kigwe, Pascal Sijila akisisitiza jambo wakati wa kikao cha mfuko huo kilichoketi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi  tarehe 08 Februari, 2019 na kupitisha majina 462 ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wamefaulu kujiunga na masomo ya Kidato cha Kwanza katika shule mbalimbali za Wilaya ya Bahi kwa mwaka 2019.




Wajumbe wa Mfuko wa Elimu Wilaya ya Bahi, wakifuatilia na kupitia mambo kwa umakini wakati wa kikao cha mfuko huo kilichoketi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi  tarehe 08 Februari, 2019 na kupitisha majina 462 ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu na wamefaulu kujiunga na masomo ya Kidato cha Kwanza katika shule mbalimbali za Wilaya ya Bahi kwa mwaka 2019. (Pisha zote na Benton Nollo).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa