• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Bahi Kinara Ujenzi Hospitali za Wilaya 67 Nchini

Imechapishwa: July 10th, 2019

Benton Nollo na Alinikyisa Humbo, Bahi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Said Jafo (Mb), amefurahishwa na kuupongeza uongozi wa Wilaya ya Bahi kwa jinsi ambavyo wamejitoa kusimamia ujenzi wa hospitali ya wilaya hiyo.

Jafo ameyasema hayo Julai 10, 2019 alipotembalea kukagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali hiyo inayojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 1.5 kwa mfumo wa “Force Account”.

Baaada ya kukagua majengo yote saba, Jafo hakusita kuonesha furaha yake mbele ya viongozi wa wilaya hiyo na kusema kuwa ujenzi unaendelea vizuri sana na alitumia fursa hiyo kuwapongeza kwa ushirikiano mzuri na hasa hatua ya kuimarisha usimamizi ya kuwagawia Wakuu wa Idara na Vitengo majengo.

“Viongozi, watendaji wote na wananchi wa Bahi mimi naomba niwapongeze katika wilaya hazizidi tano zilizonifurahisha zaidi ninyi Bahi mpo na mnawezekana katika tatu bora nyie mpo na kilichonifurahisha zaidi hii kazi mlianza kwa kuchelewa sana ukilinganisha na wilaya nyingine lakini nyie mliochelewa ndiyo mmekuwa wa kwanza zaidi, lakini siyo wa kwanza kwa vile mnamaliza tu, mmekuwa kwanza na majengo mazuri mno”. Anasema Jafo na kuongeza.

“Mimi kama Waziri wa TAMISEMI niliyepewa dhamana na Mheshimiwa Rais katika ujenzi wa hospitali 67, na sasa hivi tumeongeza nyingine 27, hospitali 94 kwa mara ya kwanza katika wilaya najivunia, Wilaya ya Bahi mmefanya kazi nzuri mno”.

Pia, Jafo alieleza kufurahishwa na utekelezaji wa agizo alilolitoa mwanzo kwa wilaya zote 67 kuwa zihakikishe katika majengo saba yanayojengwa yanakuwa na mfumo wa uvunaji wa maji ya mvua pamoja na usimikaji wa mifumo ya kielektroniki ili kurahisisha ukusanyaji wa mapato ya serikali wakati wa kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.

“Kitu kingine kilichonifurahisha zaidi kwenu, sijui katika wilaya nyingine kama wamezingatia huenda labda kwa sababu hawajamaliza, ni kwamba nimeona mmeweka gata kwa ajili ya uvunaji wa maji ya mvua kwani hili lilikuwa ni agizo langu la kwanza kwamba majengo yote yatakayojengwa lazima kusimikwe mifumo ya ukusanyaji mapato ya kielektroniki na uvunaji wa maji ya mvua hivyo naona hakuna maji yatakayopotea”. Alisema Jafo.

Hospitali ya Wilaya ya Bahi ni miongoni mwa hospitali 67 zinazojengwa na Serikali ya Awamu ya Tano nchini kwa gharama ya shilingi bilioni 1.5 na ipo katika hatua za ukamilishwaji.


Matukio katika picha:

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Said Jafo (Mb), (mwenye tai nyekundu) akitoka kukagua jengo la kuhifadhia dawa ambalo ni miongoni mwa majengo saba yanayojengwa katika ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Bahi unaoendelea. 









Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI. July 02, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE.ASHALU KIJAJI WAIZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AZINDUA CHANJO YA MIFUGO WILAYANI BAHI

    July 15, 2025
  • OFISI YA RAIS, MANAGEMENT YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA WATOA MAFUNZO YA UFANYAJI WA TATHIMINI (ASSESMENT) KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI.

    July 08, 2025
  • MHE. JOACHIM THOBIAS NYINGO AFANYA KIKAO CHA KUJADILI MIKAKATI MBALIMBALI YA MAENDELEO KUELEKEA MWAKA WA FEDHA 2025/2026 KWA IDARA MBALIMBALI NA VITENGO BAADA YA KUPOKEA BILIONI 1.7.

    July 04, 2025
  • MKURUGENZI WA MRADI WA "TUINUKE PAMOJA" CHINI AGHAKAN FOUNDATION WAKISHIRIKIANA NA TGNP ATAMBULISHA MRADI HUO KATIKA MANEJINENTI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI.

    July 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa