• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Bahi Yapata Tshs 240 Milioni Mradi wa Maji Kigwe Sekondari

Imechapishwa: March 29th, 2018

Na Benton Nollo,

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Rachel Chuwa ameuhakikishia Ubalozi wa Japan nchini Tanzania kutekeleza na kusimamia vema mradi wa usambazaji maji katika Shule ya Sekondari Kigwe uliofadhiliwa na ubalozi huo kwa shilingi 240 milioni (sawa na Dola za Kimarekani USD 110,746) kwa kuzingatia thamani ya fedha.   

Chuwa aliyasema hayo mara baada ya kusaini Mkataba wa Makubaliano kati yake na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida ubalozini Jijini Dar es Salaam tarehe 23 Machi 2018.

Ubalozi huo umetoa msaada wa fedha hizo baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kuandika andiko la mradi wa maji kwa ajili ya kutatua changamoto kubwa ya uhaba wa maji uliokuwa unaikabili shule hiyo kongwe ambayo pia ina Kidato cha Tano na Sita. 

Awali akizungumza baada ya mkataba huo kusainiwa, Balozi Yoshida alieleza kufurahishwa kwake na jitihada zilizofanywa na Halmashauri hiyo za kuandika andiko la mradi husika na kufuatilia majibu ubalozini mara kwa mara, hali iliyosababisha msaada huo kutolewa.

Balozi Yoshida alieleza kuwa fedha hizo zitatumika kujenga tenki moja lenye ujazo wa lita elfu 45 kwa ajili ya kuhifadhia maji, vituo 5 vya kutekea maji, usambazaji wa maji kwenye nyumba 3 za walimu, maabara 3, mabweni 2 ya wanafunzi, ufungaji wa mitambo ya kusukuma maji kwa kutumia nguvu ya jua, usambazaji wa mabomba kutoka kisimani hadi kwenye tenki na ujenzi wa uzio kwenye eneo la nyumba ya mashine.

Akiongea kwa njia ya simu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kigwe, Mwasiti Msokola ameelezwa kufurahishwa na msaada huo kwani utakuwa mkombozi kwa walimu, wanafunzi na jamii inayozunguka shule hiyo pamoja na kuokoa fedha nyingi zilizokuwa zikitumika kwa huduma ya maji shuleni hapo.

“Kwa kweli kwa niaba ya walimu na wanafunzi, ninayofuraha kubwa shule yetu kupatiwa msaada huo kwani tumekuwa tukitumia shilingi 400,000.00 kila mwezi kupata huduma ya maji hapa shuleni ambapo pamoja na kulipa fedha hizo katika Chombo cha Watumiaji Maji Kijiji cha Kigwe, maji hayo yalikuwa hayatoshelezi mahitaji ya walimu na wanafunzi hasa katika vyoo”. Alisema Msokola na kuongeza;

“Kwa shule yetu kupata msaada huo tutaweza kuboresha mandhari ya shule pamoja na kuanzisha miradi midogo midogo ya kilimo cha bustani za mboga mboga kupitia klabu za wanafunzi”.

Kwa upande wake Abraham Epimack Mlutee, Mwanafunzi wa Kidato cha Sita mchepuo wa HGK shuleni hapo, alieleza furaha yake kwamba huduma hiyo ikikamilika itawapunguzia adha ya kutumia muda mwingi kutafuta maji hali iliyokuwa ikiwasababishia kupoteza muda wa masomo.

“Kwa kweli nimefurahi sana tena sana kaka kwa sababu adha hii ni ya muda mrefu kwani tumekuwa tukitumia muda mwingi kutafuta huduma ya maji pindi yanapokatika na hata muda wa masomo kutupita”. Alisema Mlutee na kuongeza kwamba;

“Nakumbuka mwezi Machi, 2016 ulitokea mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu hapa shuleni na mwalimu mmoja na baadhi ya wanafunzi walikumbwa na ugonjwa huo ambapo kwa undani sababu kubwa ya kutokea mlipuko huo ni ukosefu wa maji safi na salama hapa shuleni. Hivyo, tunapopata taarifa za msaada huo tunafurahi na tunaamini mradi huo ukikamilika hata milipuko ya magonjwa kama kipindupindu hayatatokea”.         

Shule ya Sekondari Kigwe ipo Kijiji cha Kigwe, Kata ya Kigwe na ni moja kati ya shule za sekondari 20 zilizopo Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma. Katika Wilaya ya Bahi shule hiyo ni kongwe kwani ilianzishwa tarehe 16 Mei 1992 na mwaka 2011 ilipewa hadhi ya kuwa na wanafunzi wa Kidato cha Tano.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa