• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Munkunda Awaongoza Wananchi Kupata Chanjo ya UVIKO 19

Imechapishwa: August 5th, 2021

Benton Nollo na Bernard Magawa, Bahi

Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi Munkunda amezindua zoezi la Chanjo ya UVIKO 19 wilayani humo na kutoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuchanjwa ili kuwa salama dhidi ya maradhi hayo hatari.

Akizungumza kabla ya uzinduzi huo uliofanyika kiwilaya tarehe 5 Agosti 2021 katika Hospitali ya Wilaya ya Bahi na baadaye kuwa wa kwanza kupata chanjo hiyo, Mkuu huyo wa Wilaya amewaasa wananchi kupuuza upotoshaji unaoendelea katika mitandao ya kijamii kuhusiana na chanjo ya UVIKO 19 kwani hauna ukweli wowote kwa sababu wote wanaopotosha siyo wataalamu wa afya, hivyo wafike kwa wingi katika vituo vilivyoainishwa na Serikali ili kuchanjwa.

“Niwaombe Viongozi wenzangu wa dini na Serikali, tuhamasishe wananchi na Waumini wetu wafike vituoni kwa wingi kupata chanjo.” Amesema Munkunda.

Awali, akitoa taarifa ya ugonjwa huo, Mganga Mkuu Wilaya ya Bahi Dkt. Phillipina Philipo amesema wilaya hiyo imepata wagonjwa watano wenye matatizo ya upumuaji ambapo baada ya vipimo wagonjwa watatu kati ya hao watano wamegundulika kuwa na ugonjwa wa UVIKO 19 huku majibu ya wagonjwa wawili yakiwa bado hayajarudi kutoka maabara.

“Katika kukabiliana na ugonjwa huu tumeandaa vifaa tiba na dawa katika vituo vyetu vyote vya kutolea huduma za afya ikiwemo mitungi ya gesi ili kurahisisha matibabu kwa wagonjwa watakao bainika na tatizo hilo. Pia, tunahimiza maeneo yote ya biashara, shule, taasisi mbalimbali na maeneo yote ya mikusanyiko kuwa na maji tiririka kwa ajili ya kunawa mikono pamoja na uvaaji wa barakoa ili kujikinga na janga hili.” Amesema Dkt. Philipina.

Hata hivyo, Dkt. Phillipina amewatoa hofu na kuwahakikishia wananchi wilayani Bahi kuwa chanjo hiyo ni salama kwa matumizi ya binadamu na imethibitishwa na taasisi za kitaifa na kimataifa zinazohusika na sekta ya afya.

Dkt. Phillipina amesema kwamba Wilaya ya Bahi imepokea chanjo Dozi 3,000 ambapo mpaka sasa tayari watu 36 wameshachanjwa na amevitaja vituo vya kutolea chanjo hiyo wilayani Bahi kuwa ni Hospitali ya Wilaya, Kituo cha Afya Mundemu na Kituo cha Afya Chipanga.

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa dini walioshiriki uzinduzi huo, Ramadhani Issah ameipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuwajali wananchi wake na kuwaletea chanjo hiyo ambayo itawakinga na kuwalinda dhidi ya UVIKO 19 na amewasihi viongozi wenzake wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutoa elimu ya kujikinga na ugonjwa huo ambao umeitikisa dunia na kugharimu maisha ya watu.

Naye, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bahi, Sterwat Masima akizungumza katika hafla hiyo ya uzinduzi ameipongeza Serikali ya awamu ya sita kwa ujasiri na uthubutu katika kuhakikisha inaokoa Wananchi wake katika janga hilo kwa kuwaletea chanjo na kuahidi kuhamasisha wanachama wote wa chama chake kupata chanjo ili wawe salama.


Matukio katika Picha:

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (aliyevaa kilemba chekundu) pamoja na viongozi mbalimbali wilayani humo wakichomwa Chanjo ya UVIKO 19 katika hafla ya uzinduzi wa chanjo hiyo iliyofanyika Hospitali ya Wilaya ya Bahi tarehe 05 Agosti 2021. 

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (kulia) akizundua rasmi zoezi la Chanjo ya UVIKO 19 kwa hiari katika hafla ya uzinduzi wa chanjo hiyo iliyofanyika Hospitali ya Wilaya ya Bahi tarehe 05 Agosti 2021. 

Viongozi na watumishi mbalimbali wilayani Bahi wakifuatilia matukio wakati wa zoezi la uzinduzi wa Chanjo ya UVIKO 19 katika hafla ya uzinduzi wa chanjo hiyo iliyofanyika Hospitali ya Wilaya ya Bahi tarehe 05 Agosti 2021. (Picha zote na Benton Nollo).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa