• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Dkt. Mahenge: Uzeni Ufuta Mahali Popote

Imechapishwa: June 24th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge amewaruhusu wakulima wa zao la Ufuta mkoani humo ambao bado wana ufuta nyumbani, kuuza mahali popote ambapo wanaona watapata bei ya kuwafaa.

Dkt. Mahenge ametoa maelekezo hayo ya Serikali akiwa wilayani Bahi ambapo aliwatembelea Wakulima na Wafanyabiashara wadogo wa zao hilo baada ya wakulima hao kuiomba Serikali kuingilia kati bei ya zao hilo kufuatia kuporomoka kwa bei katika mnada ulioendeshwa tarehe 24 Juni 2020 kutoka bei ya shilingi 1,931 mnada wa tarehe 02 Juni 2020 hadi shilingi 1,250.   

“Maelekezo yangu baada ya kukaa kikao juzi Jumapili na Wafanyabiashara na Wakuu wa Wilaya wote ni kwamba kuanzia sasa, mwananchi yeyote ambaye bado ana ufuta nyumbani aende akauze anakoona yeye inafaa, hakutakuwa tena na hii zuia zuia isipokuwa tu utatulipia ushuru wetu kwenye geti, mmenielewa ndugu zangu”.  Amesema Dkt. Mahenge na kuongeza kuwa;

“Waambieni na wananchi wote kwamba muda uliobaki Serikali imeamua kuwaachia wananchi wafanye juhudi zake, kama unamuuzia mfanyabiashara muuzie kama unapeleka mwenyewe mjini peleka, lakini kama ipo chini ya tani moja unapeleka bila malipo ikizidi tani moja unalipa ushuru”.

Dkt. Mahenge amewaeleza wakulima hao kuwa zipo sababu tatu ambazo kimsingi ndizo zilizosababisha kushuka kwa kasi kwa bei ya zao ufuta katika mkoa wa huo kuwa ni athari za Ugonjwa wa Corona ambapo wanunuzi wakubwa duniani bado nchi zao hazijafungua mipaka yao hivyo imekuwa vigumu kupeleka ufuta katika nchi hizo.

Sababu ya pili, Dkt. Mahenge ameitaja kuwa Mkoa wa Dodoma huwa wa kwanza kuanza kuvuna ufuta lakini kutokana na mvua nyingi zilizonyesha mwaka huu (2020) mavuno yalichelewa kuanza na wakulima wakajikuta wanaanza kuvuna mwezi Mei na Juni ilhali mikoa ya kusini nayo ndiyo msimu wa kuvuna zao hilo na hata katika nchi za Malawi na Ivori Coast nazo ndiyo msimu wa mavuno hivyo, kufanywa ufuta kuwa mwingi sokoni.

Dkt. Mahenge ameainisha sababu ya tatu ya kushuka kwa bei ya zao hilo kuwa katika msimu wa kilimo wa mwaka 2020 uzalishaji wa ufuta ulikuwa mkubwa kwani wakulima wamevuna vizuri kwa kuwa mvua zimenyesha vizuri na za kutosha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amemueleza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuwa katika mnada uliofanyika tarehe 24 Juni 2020 kwa dakika 15 wilaya hiyo ilikuwa na tani 78.2 ambapo bei ya mnunuzi aliyejitokeza alinunua kwa shilingi 1,250 kwa kilo moja jambo ambalo halikuwaridhisha wakulima na kuamua kutouza shehena hiyo.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwa kuona kuwa tumeshafanya minada miwili na huu wa leo ni wa tatu na bei haituridhishi kwa sababu tulianza na bei ya 1,820 tulikataa, tukaja 1, 520 nayo tulikataa na hii ya leo ya shilingi 1,250 imekuwa mbaya zaidi…hivyo, kama kiongozi baada ya kuona hali inakuwa mbaya nikaamua kuchukua hatua kwa kushirikiana na wakulima kutafuta mnunuzi nje ya mnada na ambapo tumempata na atachukua mzigo huo kwa shilingi 1,400 na wakulima wameridhia”. Amesema Munkunda.

Naye Tito Chifungo, ambaye ni mkazi na mkulima wa ufuta katika Kijiji cha Mundemu ameishukuru Serikali na kuridhika na jitihada ilizochukua katika kushughulikia suala hilo hali ambapo kwa niaba ya wakulima wenzie wameridhishwa na uamuzi wa Serikali kuwaruhusu kuuza zao hilo mahali popote wanapopataka.

 Zao la Ufuta katika Mkoa wa Dodoma ni kwa mara ya kwanza katika msimu wa kilimo wa mwaka 2019/2020 liliingia katika Mfumo wa Stakabadhi Ghalani.

Pichani ni Zao la Ufuta unaolimwa wilayani Bahi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge (wa kwanza kushoto) akizungumza na wakulima wa Ufuta katika Ghala la Bahi ambalo limekuwa likitumika katika uuzaji wa zao hilo kwa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani alipotembelea na kuzungumza nao tarehe 24 Juni 2020. Dkt. Mahenge amewaruhusu wakulima wa zao hilo mkoani humo ambao bado wana ufuta nyumbani, kuuza mahali popote ambapo wanaona watapata bei ya kuwafaa kutoka na kushuka kwa bei ya zao hilo na kuwaathiri wakulima.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda katikati) akimueleza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge (wa kwanza kushoto) hali halisi juu ya mwenendo wa uuzaji wa zao la ufuta kwa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani wilayani humo pamoja na changamoto zake. Dkt. Mahenge amewaruhusu wakulima wa zao hilo mkoani humo ambao bado wana ufuta nyumbani, kuuza mahali popote ambapo wanaona watapata bei ya kuwafaa kutoka na kushuka kwa bei ya zao hilo na kuwaathiri wakulima. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa