• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii Yashauriwa Kuacha Ukatili

Imechapishwa: December 17th, 2020

Na Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi

Wito umetolewa kwa Wananchi wa Wilaya ya Bahi kuhakikisha wanaitumia vema ofisi ya Dawati la Jinsia na Watoto ili kupunguza ukatili kwa wanawake na watoto.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda wakati wa uzinduzi wa kituo kipya cha Dawati la Jansia na Watoto kilichojengwa kwa ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wanawake (UN WOMEN) katika ofisi ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi tarehe 17 Desemba 2020.

Munkunda amelipongeza Jeshi la Polisi wilayani humo kwa utendaji mzuri hususan katika kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na makosa ya kijinsia yanayolipotiwa ambapo takwimu zinaonesha kwa mwaka 2019/2020 zaidi ya kesi 60 zilisikilizwa na kupatiwa hukumu.

“Ukatili wa kijinsia una athari kubwa sana katika ukuaji wa uchumi, mtu aliyeathirika kijinsia hawezi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi kwani anakosa kujiamini.” Amesema Munkunda na kuongeza;

“Niwaombe maofisa mtakaofanya kazi katika dawati hili msikae ofisini kusubiri kesi, zifuateni mitaani kwa maana watanzania tulivyolelewa siyo watu wa kesi kesi. Hivyo, andaeni vipindi mbalimbali vya kuelimisha katika shule na maeneo mengine ili waweze kuipata elimu hii.”

Awali akizungumza kabla ya uzinduzi wa jengo hilo, Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Bahi, Mrakibu wa Polisi Idd Ibrahimu amesema tayari watumishi sita wameshapatiwa mafunzo kwa ajili ya uendeshaji wa ofisi hiyo.

Naye, Mratibu wa Dawati la Jinsia na Watoto Tanzania, Naibu Kamishana wa Polisi Mary Nzuki amesema tangu dawati hilo lianzishwe hapa nchini mwaka 2008 tayari madawati 400 yameshaanzishwa nchini ambapo ameiomba jamii kushirikiana na serikali kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la UN WOMEN, Hodan Addouh amesema wao kama wadau wa maendeleo wanatambua kwa dhati thamani ya ushirikiano wanaoupata kutoka kwa Jeshi la Polisi na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika kutekeleza Mpango wa Taifa wa kupambana na ukiukwaji wa haki za wanawake na watoto.

 Aidha, pamoja na kufadhili ujenzi wa jingo hilo, Shirika la UN WOMEN pia limetoa samani zenye thamani ya shilingi milioni 10.7.


Matukio katika picha wakati wa uzinduzi wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Bahi.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza katika hafra ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Bahi.

Mratibu wa Dawati la Jinsia na Watoto Tanzania, Naibu Kamishana wa Polisi Mary Nzuki akizungumza katika hafra ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Bahi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Bahi, Mrakibu wa Polisi Idd Ibrahimu akizungumza katika hafra ya uzinduzi wa Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Bahi.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa