• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Jamii Yatakiwa Kushirikiana, Serikali Kubaini Walengwa Wenye Uhitaji

Imechapishwa: July 29th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umeitaka jamii kushirikiana na Serikali katika kuwabaini na kuwatambua Wananchi wenye uhitaji ili kuondoa udanganyifu katika utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF III) Awamu ya Pili unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Wito huo umetolewa Julai 29, 2020 na Mtaalam wa Utafiti na Maendeleo wa TASAF, Tumpe Lukongo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kutoa mafunzo kwa Wakuu wa Idara na Wawezeshaji wa Ngazi ya Halmashauri, Wilaya ya Bahi kuhusiana na zoezi la uhakiki wa Walengwa wa kaya maskini.

Lukongo amesema TASAF III Awamu ya Kwanza imeisha na sasa wapo katika utekelezaji wa TASAF III Awamu ya Pili ambapo kwa sasa wanafanya uhakiki wa wanufaika ili kupata masijala safi ya walengwa kabla ya kuanza utekelezaji wa mpango huo.

“Rais Dkt. John Magufuli wakati anazindua TASAF III Awamu ya Pili alituelekeza kwamba kabla hatujaanza utekelezaji tufanye, uhakiki na kusafisha Daftari la Kaya Maskini ili tuwapate walengwa wanaostahili na tulishaanza kutekeleza maelekezo hayo nchi nzima na sasa tunamalizia Mkoa wa Dodoma, Singida, Kigoma, Lindi na Mtwara". Alisema Lukongo.

Amesema ili zoezi hilo lifanikiwe kwa ufanisi ni muhimu Wananchi washirikiane na Serikali katika ngazi zote, kinyume na hapo jitihada za serikali za kuondoa umaskini zinaweza zisifike kwa walengwa.

“Jamii ndio inamjua mtu maskini, inamjua mtu anayehitaji msaada zaidi ya wengine, hivyo ikishirikiana na serikali kwa ukweli na uwazi itasaidia kuondoa changamoto ya udanganyifu ambayo imekuwepo katika baadhi ya maeneo.” Aliongeza Lukongo.

Amesema lengo la uhakiki huo ni kuwa na orodha halisi ya walengwa kwenye masijala ya kaya za walengwa kwa kuondoa waliofariki, aliyehama, kiongozi wa kijiji, kaya ya mjumbe wa kamati ya usimamizi wa jamii na kaya ambayo haikufika kuchukua malipo yake mara mbili mfululizo.

Ili kuondoa changamoto ya udanganyifu amesema wameboresha dodoso la utambuzi na namna ya udodosaji ambapo mwanzo walikuwa wanatumia wahusika ngazi ya jamii lakini kwa sasa wanatumia wawezeshaji ngazi ya Halmashauri ambao wanapewa mafunzo ya kutumia vishkwambi kuingiza taarifa badala ya makaratasi.

 Ametaja mafanikio yaliyofikiwa katika utekelezaji wa TASAF III Awamu ya Kwanza, kuwa ni pamoja na maisha ya walengwa kuboreka, walengwa wengi kujishughulisha na shughuli za kuongeza kipato, kupata uwezo wa kusomesha watoto wao, kuboresha afya na lishe.

Kiongozi wa Timu ya Uhakiki ya TASAF, Abasi Salehe akizungumza wakati  wa Mafunzo ya kujenga uwezo kuhusu kipindi cha pili cha TASAF III na uhakiki wa Kaya kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wawezeshaji Ngazi ya Halmashauri tarehe 29 Julai 2020.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Denis Komba akisisitiza jambo wakati  wa Mafunzo ya kujenga uwezo kuhusu kipindi cha pili cha TASAF III na uhakiki wa Kaya kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wawezeshaji Ngazi ya Halmashauri tarehe 29 Julai 2020.

Mratibu wa TASAF Wilaya ya Bahi, Joseph Kileo akizungumza wakati  wa Mafunzo ya kujenga uwezo kuhusu kipindi cha pili cha TASAF III na uhakiki wa Kaya kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wawezeshaji Ngazi ya Halmashauri tarehe 29 Julai 2020.

Afisa Ufuatiliaji wa TASAF Wilaya ya Bahi, Amani Christian akizungumza wakati  wa Mafunzo ya kujenga uwezo kuhusu kipindi cha pili cha TASAF III na uhakiki wa Kaya kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wawezeshaji Ngazi ya Halmashauri tarehe 29 Julai 2020.

Baadhi ya Washiriki wakifuatilia kwa makini Mafunzo ya kujengewa uwezo kuhusu kipindi cha pili cha TASAF III na uhakiki wa Kaya yaliyofanyika kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wawezeshaji Ngazi ya Halmashauri tarehe 29 Julai 2020 kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.

Mwezeshaji wa Mafunzo kutoka TASAF, Grace Kibonde akitoa maelezo kuhusu Kipindi cha Pili cha Mpango wa TASAF III  kwa Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wawezeshaji Ngazi ya Halmashauri tarehe 29 Julai 2020 kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.


Mwezeshaji wa Mafunzo kutoka TASAF, Grace Kibonde (wa kwanza kushoto) akiwaelekeza washiriki wa Mafunzo namna ya kutumia Vishkwambi kwa ajili ya zoezi la uhakiki wa Walengwa wa Kaya Maskini katika Halmashaurinya Wilaya ya Bahi tarehe 29 Julai 2020. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa