• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kamati ya Ujenzi Yaagizwa Kusimamia Madarasa

Imechapishwa: December 1st, 2020

Na  Benton Nollo na Bernard Magawa DMC, Mundemu

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda ameiagiza Kamati ya Ujenzi ya Shule ya Sekondari Mundemu kukamilisha haraka ujenzi wa majengo inayoyasimamia kabla ya mwezi Januari 2021 ili yaweze kutumiwa na wanafunzi wa Kidato cha Kwanza 2021.

Munkunda ameyasema hayo tarehe 01 Desemba 2020 alipotembelea shuleni hapo kukagua maendeleo ya ujenzi wa madarasa mawili, bweni moja na choo chenye matundu 8 ambapo Serikali kupitia programu ya Lipa Kulingana na Matokeo – EP4R imetoa shilingi milioni 128.6 kujenga majengo hayo.

“Mmepata bahati ya kupokea fedha za ujenzi shuleni kwenu, hakikisheni mnakamilisha mapema ili watoto wa Kidato cha Kwanza watakapochaguliwa kujiunga na masomo shuleni hapa wakute majengo haya yapo tayari kwa matumizi.” Amesema Munkunda.

Munkunda baada ya kukagua majengo hayo ameipongeza kamati hiyo kwa usimamizi mzuri unaozingatia viwango vya ujenzi wa majengo ya serikali na thamani ya fedha inaonekana.

Aidha, Munkunda ameiagiza kamati hiyo kuhakikisha kuwa inaongeza kasi ya ujenzi kwa kuwasimamia mafundi kwa karibu na kwamba ifikapo tarehe 20 Desemba 2020 majengo yote yawe yamekamilika ili watoto watakao chaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza 2021 shuleni hapo waweze kuyatumia.

Awali akisoma taarifa za maendeleo ya ujenzi wa majengo hayo Mkuu wa Shule hiyo, Reubeni Nchimbwi amesema mwezi Juni 2020 shule yake ilipokea fedha hiyo lakini utekelezaji ulichelewa kuanza kutokana na kufungwa kwa mifumo ya Serikali baada ya mwaka wa fedha 2019/2020 kuisha.  

Naye, Diwani Mteule wa kata hiyo, Msafiri Mtati amesema kata yake imejipanga kuhakikisha majengo hayo yanakamilika kwa wakati na wameandaa mkakati maalum wa usimamizi.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (aliyevaa kilemba) akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ujenzi ya Shule ya Sekondari Mundemu (hawapo pichani) katika ziara yake aliyoifanya tarehe 01 Desemba 2020.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (aliyevaa kilemba) akikagua ujenzi wa miundombinu unaoendelea Shule ya Sekondari Mundemu katika ziara yake aliyoifanya tarehe 01 Desemba 2020.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mundemu, Reuben Nchimbwi akisoma taarifa ya ujenzi wa bweni moja, madarasa mawili na choo chenye matundu 8 unaoendelea shuleni hapo katika ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi (hayupo pichani) aliyoifanya tarehe 01 Desemba 2020.

Diwani Mteule wa Kata ya Mundemu, Msafiri Mtati akiishukuru Serikali kwa kutoa shilingi milioni 128.6 kwa ajili ya ujenzi  wa bweni moja, madarasa mawili na choo chenye matundu 8 katika Shule ya Sekondari Mundemu jambo ambalo litawasaidia wanafunzi wa Kidato cha Kwanza mwaka 2021. Mtati ametoa shukrani hizo katika ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi (hayupo pichani) aliyoifanya tarehe 01 Desemba 2020. (Picha zote na Benton Nollo).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa