• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Luteni Mwambashi Apongeza Ujenzi wa Madarasa Bahi Sekondari

Imechapishwa: July 25th, 2021

Benton Nollo na Bernard Magawa

Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru 2021, Luteni Josephine Mwambashi ameipongeza Kamati ya Ujenzi ya Shule ya Sekondari Bahi kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa pamoja na miundombinu ya TEHAMA ambapo thamani ya fedha imeonekana.

Luteni Mwambashi ameyasema hayo tarehe 25 Julai 2021 ambapo Mwenge wa Uhuru ulifika shuleni hapo kwa ajili ya uzinduzi wa jengo hilo ambalo limejengwa kwa fedha za Serikali kupitia Programu ya Lipa Kulinga na Matokeo EP4R Awamu ya Tisa 2021.

Akizungumza baada ya kukagua jengo hilo pamoja na miundombinu ya TEHAMA, ameipongeza Kamati ya Ujenzi hasa kwa kujiongeza na kujenga ofisi ya walimu katikati licha ya kwamba ramani ya wizara haikuwa na ofisi ya walimu hivyo, kwa kufanya hivyo wametatua changamoto ya uhaba wa ofisi kwa walimu shuleni hapo na ameagiza madarasa hayo yatunzwe ili yaweze kuwanufaisha wanafunzi katika kujifunza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amemshukuru Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021 kwa kuridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kuuzindua rasmi.

“Mradi huu utakuwa chachu kwa Wanafunzi wetu kujifunza TEHAMA kwa vitendo wawapo shuleni hapa, nikuhakikishie Ndugu Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kuwa majengo haya pamoja na miundombinu yake vitatunzwa vizuri na ninafurahi kukutaarifu kuwa katika Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huu wa 2021 wanafunzi wetu watafanya kwa vitendo mtihani wa taifa wa somo la TEHAMA kwanza mara ya kwanza.” Amesema Munkunda.

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021, Mkuu wa Shule ya Sekondari Bahi, Eliakimu Solomoni amesema mradi huo umegharimu shillingi milioni 58 hadi kukamilika kwake ambapo kati ya hizo shilingi milioni 40 zimetolewa na Serikali na shilingi milioni 18 zimetolewa na wahisani pamoja na nguvu ya wananchi.

“Ndugu kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru kitaifa, lengo la mradi huu ni kuwawezesha wanafunzi kupata stadi na ujuzi wa kutumia mfumo wa Teknolojia katika ufundishaji na ujifunzaji wa masomo hasa kufanya majaribio kwa vitendo.” Amesema Solomoni.

 Wilaya ya Bahi imekuwa ya kwanza katika Mkoa wa Dodoma kuanza kukimbisa Mwenge wa Uhuru 2021 ukitokea Wilaya ya Manyoni mkoani Singida.


Matukio Katika Picha:

Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021, Luteni Josephine Mwambashi akizungumza kabla ya kuzindua jengo la madarasa mawili, ofisi ya walimu na miundombinu ya TEHAMA katika Shule ya Sekondari Bahi tarehe 25 Julai 2021.

Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021, Luteni Josephine Mwambashi (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (kulia) aliyekuwa akimshukuru kiongozi huyo baada ya kuzindua jengo la madarasa mawili, ofisi ya walimu na miundombinu ya TEHAMA katika Shule ya Sekondari Bahi tarehe 25 Julai 2021.

Muonekano wa jengo la madarasa mawili na ofisi ya walimu lililozinduliwa na Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021 tarehe 25 Julai 2021 ambalo ujenzi wake umegharimu shilingi milioni 58 ambapo kati ya hizo shilingi milioni 40 zimetolewa na Serikali kupitia Programu ya Lipa Kulingana na Matokeo - EP4R Awamu ya Tisa 2021 na shilingi milioni 18 zimechangiwa na Wahisani na Nguvu za Wananchi.

Mwenge wa Uhuru 2021 ukiwasili Shule ya Sekondari Bahi tarehe 25 Julai 2021.

Wakimbiza Mwenge Maalum wa Uhuru Kitaifa 2021 wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Mwenge huo kukabidhiwa wilayani Bahi katika Kijiji cha Uhelela tarehe 25 Julai 2021. Kutoka kushoto ni Luteni Ramadhani Ally Msham, Koplo Rehema Ali Haji, Private Dismas Egno Mvula, Luteni Mussa Hassan Mussa na Luteni Geofrey Jume Aron.


Picha za juu ni mapokezi ya Mwenge wa Uhuru 2021 Kijiji cha Uhelela tarehe 25 Julai 2021. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa