• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mejiti: Sasa ni Uamsho wa Matoleo

Imechapishwa: January 19th, 2021

Na Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi

Wananchi wilayani Bahi mkoani Dodoma wamehimizwa kujitolea nguvu kazi katika miradi mbalimbali ya maendeleo inayopelekwa na Serikali ili kuifanya ikamilike kwa wakati badala ya kuiachia serikali ifanye kila kitu wakati wanufaika wakuu wa miradi hiyo ni wananchi wenyewe.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Donald Mejiti katika ziara ya Ukaguzi wa Miradi iliyoifanywa kwa siku mbili (tarehe 18 na 19 Januari 2021) na wajumbe wa Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango (FUM).

“Kuanzia leo tukiletewa mradi wowote na Serikali, lazima wananchi washiriki katika kazi mbalimbali kama vile kuchimba msingi, kumwaga zege, kusogeza udongo, mchanga, matofali na kazi zote za mikono, hatuwezi kuiachia serikali ifanye kila kitu wakati wanufaika wakuu wa miradi hii ni sisi wananchi wenyewe.” Amesema Mejiti na kuongeza:

“Hiki ni kipindi cha kufanya kazi, viongozi na watendaji tusimamie maendeleo kikamilifu na kuhakikisha wananchi wetu wanashirikI kwa wingi katika kutekeleza miradi kwa kujitolea nguvu kazi.

Miradi iliyokaguliwa na Kamati hiyo ni ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa Shule Shikizi ya Lioni, vyumba viwili vya madarasa Shule Shikizi ya Suguta, Shule Shikizi ya Mzogole na Shule Shikizi ya Sanza iliyopo Kijiji cha Mpalanga.

Miradi mingine ni ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, bweni la wavulana na choo chenye matundu 8 Shule ya Sekondari Mundemu, ujenzi wa Zahanati ya Chidilo, na ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa, bweni la wavulana na choo chenye matundu 8 Shule ya Sekondari Nondwa na ujenzi wa njia za kutembelea Kituo cha Afya Mundemu zinazojengwa kwa ufadhili wa Shirika la World Vision Tanzania.

Awali, akitoa taarifa ya ujenzi katika kijiji cha Mpalanga kwa Madiwani, Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Maria Dominick amesema ushiriki wa jamii katika miradi hiyo ni mdogo na kuomba uongozi wa juu kuwasaidia kuelimisha wananchi ili washiriki kikamilifu katika miradi hiyo kupitia nguvu kazi ili waweze kuokoa fedha ambazo zinaweza kufanya kazi nyingine za maendeleo.

 Akizungumza katika ziara hiyo, mjumbe wa kamati hiyo Arois Sokozi amewahimiza viongozi katika ngazi za vijiji na kata kushikamana na kushirikiana kwa pamoja katika kusimamia miradi hiyo ili kuwa na ufanisi zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa