• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Milioni 83 Zakopeshwa kwa Wajasiriamali

Imechapishwa: January 20th, 2021


Na Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi 

Halmashauri ya Wilaya ya Bahi imetoa mikopo kwa vikundi 25 vya wajasiriamali wadogo wadogo yenye thamani ya shilingi milioni 83.1 ambayo ni asilimia 10 ya makusanyo yake ya ndani kwa mujibu wa sheria.

Mikopo hiyo yenye lengo la kuwasaidia wajasiriamali kukuza mitaji na kuongeza vipato vyao ili waweze kujikwamu na umaskini, imetolewa Makao Makuu ya Halmashauri hiyo tarehe 20 Januari 2021.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi mikopo hiyo mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda ameishauri kwamba pamoja na kuwakopesha fedha hizo pia, Halmashauri itoe kipaumbele kwa wajasiriamali hao katika shughuli mbalimbali zinazotokea kama vile huduma za chakula katika mikutano na matukio mbalimbali badala ya kuwapa kazi hizo watu kutoka maeneo mengine ili kuwajengea uwezo wa kurejesha kwa wakati mikopo hiyo.

“Serikali ya awamu ya tano imejipanga kuwasaidia wanyonge mkiwemo ninyi wajasiriamali, tunatamani kila kijana wa Bahi awe na kazi ya kufanya hivyo niwaombe muwe mabalozi wazuri katika zoezi la ukusanyaji wa ushuru mbalimbali ili asilimia kumi ya mapato hayo iendelee kurudi kwenu na kuwafikia wengi zaidi.” Amesema Munkunda na kuongeza:

“Niwaombe mliokopeshwa jengeni utamaduni wa kurejesha kwa wakati ili fedha hizi ziendelee kuzunguka na kunufaisha wengi zaidi, na ambao hawatarejesha mikopo tutawashughulikia kama wanavoshughulikiwa wahujumu uchumi kwani utakuwa umeihujumu Halmashauri na wananchi wote kwa sababu fedha hizo zinapaswa kuzunguka kwenda kwenye vikundi vingine na siyo kubaki kwenye kikundi kimoja.”

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Donald Mejiti amewashauri wajasiriamali hao kujiunga na Mfuko wa Afya wa Jamii Iliyoboreshwa (CHF) ili kujihakikishia matibabu pindi wanapougua na kupunguza gharama za matibabu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Bahi Dkt. Fatuma Mganga amewaasa wajasiriamali hao kutafuta fursa ili waweze kuinua vipato vyao kwa haraka badala ya kubaki wakisubiri ziwafikie mahali walipo.

 Awali akitoa taarifa kwa Mgeni rasmi, Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Bahi, Denis Komba amesema vikundi 33 vimehudhuria. Ambapo kati ya hivyo vikundi vilivyopewa mikopo ni 25 vikijumuisha wanawake, vijana na wenye ulemavu ambavyo vinajishughulisha na ufugaji, mama ntilie, ushonaji wa nguo, kilimo cha mbogamboga na matunda pamoja na boda boda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa