• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Munkunda: Lishe Bora Muhimu kwa Afya ya Jamii

Imechapishwa: June 22nd, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amesema ili jamii iweze kushiriki vema katika shughuli mbalimbali za maendeleo ni lazima iwe na afya njema, ambayo  hupatikana kwa mtu kuwa na lishe bora.

Munkunda ameyasema hayo wakati anafunga kikao cha kujadili utekelezaji wa maazimio ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 pamoja na taarifa ya Lishe kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2020 kilichoketi Bahi tarehe 22 Juni 2020.

Mkuu huyo wa Wilaya amewapongeza Wataalam wa Afya wanaotoa huduma vituoni na Watoa Huduma Ngazi ya Jamii kwa kushirikiana vema na Jukwaa la Lishe Tanzania - PANITA kupitia Mradi wa Lishe Endelevu, wameweza kutekeleza Afua tisa (9) za mkataba huo kwa asilimia 81.7 katika kipindi hicho.

"Suala la lishe katika Wilaya ya Bahi ni miongoni mwa vipaumbele vyetu kwani tunaamini ili jamii iweze kushiriki vema katika shughuli za kujiletea maendeleo na kukuza uchumi ni lazima iwe na afya njema na Afya njema inatokana na lishe bora". Anasema Munkunda.

Munkunda amesema kuwa hata tarehe 29 Juni 2020 shule zitakapofunguliwa, wilaya imeweka mkakati wa kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula shuleni ili waweze kumudu vizuri masomo yao.

Pia, Munkunda ametoa wito kwa akina mama wajawazito kutumia vidonge vya kuongeza damu lakini pia Wataalam wa Afya waendelee kutoa unasihi wa lishe  kwa wazazi au walezi wa watoto wenye umri kati ya miezi 0 hadi 23.

Kadhalika, amewasihi kuèndelea kutoa matone ya Vitamini 'A' kwa watoto wenye umri  wa  miezi 6 hadi 59.

Munkunda pia, amewahimiza Wataalam hao kuendelea kuwaibua watoto wenye utapiamlo mkali ili waweze kupatiwa matibabu.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Dkt. Philipina Philipo ameushukuru Uongozi wa Jukwaa la Lishe kwa kushirikiana vema na Wilaya ya Bahi kutekeleza maazimio ya Mkataba wa Lishe.

 Naye Mkurugenzi wa Mtendaji wa PANITA, Tumaini Mikindo ameupongeza Uongozi wa Wilaya ya Bahi kwa kutekeleza maazimio hayo na ameiomba Halmashauri kuendelea kufanya ukaguzi wa vyakula katika maeneo ya biashara na kutoa fedha kupitia mapato ya ndani kutekeleza shughuli za lishe.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Dkt. Philipina Philipo akizungumza wakati kikao cha kujadili utekelezaji wa maazimio ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 pamoja na taarifa ya Lishe kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2020 kilichoketi Bahi tarehe 22 Juni 2020.

Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Lishe Tanzania - PANITA, Tumaini Mikindo akizungumza wakati kikao cha kujadili utekelezaji wa maazimio ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 pamoja na taarifa ya Lishe kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2020 kilichoketi Bahi tarehe 22 Juni 2020.

Mratibu wa Programu wa Jukwaa la Lishe Tanzania - PANITA, Jane Msagati akizungumza wakati kikao cha kujadili utekelezaji wa maazimio ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 pamoja na taarifa ya Lishe kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2020 kilichoketi Bahi tarehe 22 Juni 2020.

Wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilaya ya Bahi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya hiyo, Mwanahamisi Munkunda (hayupo pichani) wakati akifunga kikao cha kujadili utekelezaji wa maazimio ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 pamoja na taarifa ya Lishe kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2020 kilichoketi Bahi tarehe 22 Juni 2020.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (wa pili kushoto waliokaa), Afisa Lishe Mkoa wa Dodoma, Heriet Carin (wa pili kulia waliokaa), Mganga Mkuu Wilaya ya Bahi, Dkt. Philipina Philipo (wa kwanza kulia waliokaa) Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Lishe Tanzania (wa kwanza kushoto waliokaa) na Wajumbe wa Kamati ya Lishe Wilaya ya Bahi wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufungwa kwa kikao cha kujadili utekelezaji wa maazimio ya Mkataba wa Lishe kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2019 pamoja na taarifa ya Lishe kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2020 kilichoketi Bahi tarehe 22 Juni 2020. (Picha zote na Benton Nollo)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa