• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NEC Yamkabidhi Dkt. Magufuli Cheti cha Ushindi Nafasi ya Urais

Imechapishwa: November 1st, 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi – NEC, imemkabidhi rasmi cheti cha ushindi Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Magufuli baada ya kupata ushindi wa asilimia 84.4 katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

Cheti hicho kimekabidhiwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage Makao Makuu ya ofisi hizo Njedengwa jijini Dodoma leo tarehe 01 Novemba 2020.

Dkt. Magufuli ametumia fursa hiyo kuwashukuru Watanzania huku akiwakumbusha Watanzania kuendelea kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo.

Pia, Dkt. Magufuli amewashukuru Watanzania kwa kukipatia ushindi mkubwa chama chake cha Mapinduzi (CCM) katika nafasi ya Urais, Ubunge, Udiwani na kule Zanzibar katika nafasi ya Urais, Uwakilishi na nafasi ya Udiwani.

''Kupata asilimia 84.4 ni imani kubwa sana kwa Watanzania na nasema kwa dhati nina deni kubwa sana kwa Watanzania, imani yao nitaitimiza kwa kufanya kazi sana usiku na mchana”. Amesema Rais Mteule Dkt. Magufuli na kuongeza;

“Siasa sio vita, siasa sio ugomvi, sisi sote ni Watanzania, napenda kuwaahidi nitashirikiana nanyi katika kuhakikisha tunasukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi yetu. Tanzania kwanza mambo mengine baadaye".

Kadhalika, Dkt. Magufuli hakusita kuwashukuru viongozi wa dini ambao kwa kipindi chote cha uchaguzi waliweza kuwaongoza Watanzania kwa dua na sala na hatimaye kumaliza uchaguzi kwa usalama na taifa lao kuendelea kubaki na amani.

Aidha, Dkt. Magufuli amewashukuru wapinzani wake waliokubali matokeo akisema ''Nawashukuru na kuwapongeza kwa kukubali matokeo na kuja kushiriki hafla hii. Hii ni ishara ya kukomaa kwenu kisiasa hongereni sana. Ni kweli kwamba wananchi wametupatia ushindi mkubwa sana, lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya kudharau maoni na ushauri wenu".

Vile vile, kiongozi huyo aliendelea kutoa shukurani zake kwa kusema "Navishukuru pia vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa na kuhakikisha amani na usalama vinatawala katika kipindi chote cha uchaguzi'.

Kwa nafasi ya kipekee Dkt. Magufuli amewashukuru viongozi wa nchi nyingine waliomtumia salamu za pongezi.

Rais Mteule Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuapishwa Alhamisi tarehe 05 Novemba 2020 katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma ambapo kwa mujibu wa Msemaji Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbas aliyezungumza baada ya hafla hiyo amesema kwamba maandalizi kwa ajili ya tukio hilo yamekamilika kwa zaidi ya asilimia 99 na Serikali itaendelea kuwataarifu mara kwa mara.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  (katikati) akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi - NEC, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage (kushoto) mara baada ya kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020, hafla hiyo imefanyika Makao Makuu ya NEC Njedengwa jijini Dodoma  tarehe 01 Novemba 2020.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan (wa tatu kutoka kulia) akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Makamu wa Rais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi - NEC, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage (kushoto).

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (wa pili kushoto) akionesha Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais alichokabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi - NEC, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage (kushoto) mara baada ya kutangazwa mshindi wa nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akiwa amesimama na Waliogombea Urais kupitia vyama Mbalimbali vya Upinzani nchini wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla fupi ya kukabidhi Cheti cha Ushindi kwa Kiti cha Urais zilizofanyika Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya  Uchaguzi - NEC Njedengwa jijini Dodoma tarehe 01 Novemba 2020.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa