• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali Kuzungumza, Taasisi za Kifedha Kunusuru Wakulima wa Mpunga

Imechapishwa: May 8th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Serikali wilayani Bahi imewaahidi Wakulima wa mpunga wilayani humo kuwa ipo tayari kufanya mazungumzo na taasisi za kifedha kuona namna ambavyo wakulima hao watafanikiwa kurejesha fedha walizokopa baada ya zaidi ya ekari 11,000 za mashamba ya mpunga zilizokuwa katika hatua ya uvunaji kufunikwa na maji kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha kwenye mikoa ya jirani (Manyara na Arusha).

Mashamba yaliyokumbwa na athari hiyo ni katika Skimu za Bahi Makulu (ekari 9,000), Bahi Sokoni (ekari 2,347) na Nguvumali (ekari 371) ambapo kwa baadhi ya wakulima wanalazimika kuvuna mpunga kwa kutumia mitumbwi.

Akizungumza na Wakulima wa skimu hizo Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda aliyekuwa kaambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo amesema atashirikia na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuzungumza na benki zilizowakopesha wakulima hao ili kuona namna nzuri ambayo itawasaidia wakulima kurejesha mikopo.

“Viongozi wa AMCOS ili tulishughulikie suala hili ipasavyo ni vema sisi kama Serikali tukapata haraka orodha ya mashamba na wakulima kwa kiasi walichokopa, wamerejesha shilingi ngapi na kiasi gani bado…pia, natambua kuna baadhi ya wakulima wamekopeshwa na watu binafsi…tafadhali wasiwasumbue wananchi kwa kuwa hali halisi wanaiona na atakayewasumbua nipatiwe taarifa haraka”. Amesema Munkunda.

Munkunda ambaye alitumia usafiri wa gari, pikipiki na mtumbwi kwa takriban kilomita 20 kuwafikia wakulima hao na kujionea athari waliyoipata, amewatia moyo kwamba pamoja na athari hiyo, amewaagiza Wataalam wa Kilimo kupanga mikakati ya kuyatumia maji hayo kwa ajili ya shughuli nyingine za kilimo cha umwagiliaji hasa zao la vitunguu ambavyo kwa sasa vina soko zuri pamoja na mboga mboga kama mazao mbadala ya biashara.

“Kuvunjika kwa koleo siyo mwisho wa ujenzi…najua maisha ya wananchi wengi wa Bahi Sokoni na Bahi Makulu yamekuwa bora kutokana na kilimo cha mpunga, nafahamu mmechukua mikopo kwa ajili ya mashamba haya, tutazungumza na benki kwa kushirikiana na Mkuu wa Mkoa ili tuone namna ya kuusogeza mbele muda wa marejesho”. Amesema Munkunda.

Awali, Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika wa Kilimo na Masoko (AMCOS) Bahi Makulu, Hilary Ndugai amesema Skimu ya Bahi Makulu ni kubwa sana na yote imefunikwa na maji yaliyoletwa na Mto Bubu ambao chanzo chake ni mikoa ya Manyara na Arusha.

“Hali hii imefuta matumaini yetu wakulima wa Bahi, hasa ikizingatiwa kuwa tulichukua mikopo ili tulime na tunatakiwa kurejesha wakati wa mavuno, mpunga ulikuwa tayari umeshakomaa, tulikuwa tunasubiri tu kuvuna, lakini sasa kama mnavyoona maji ni mengi na yamefunika mpunga wote”.

Naye Makamu Mwenyekiti wa AMCOS hiyo, Ally Mahimbu, aliiomba Serikali kuzungumza na taasisi za fedha zilizowakopesha ili kutoa unafuu kwenye urejeshaji wa mikopo hiyo kutokana na kupata athari ya mvua.

“Kutokana na athari hizi za mafuriko nina uhakika kuna watu watashindwa kurejesha, tunaomba Serikali izungumze na benki kusogeza mbele utaratibu wa kurejesha kidogo kidogo hata baada ya msimu huu kuisha”. Amesema Mahimbu.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya, Mtendaji wa Kijiji cha Bahi Makulu, Lightness Swai amesema katika msimu wa kilimo wa mwaka 2019/2020 wakulima walilima ekari 9,000 za mpunga na zote zimefunikwa na maji.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mpamantwa, Sostheness Mpandu alisema msimu wa kilimo uliopita wakulima walipata hasara kutokana na kupata mvua chache, na mwaka huu walijipanga na kulima tena kwa kuwa mvua zilikuwa nyingi na za kutosha lakini mwaka huu (2020) wamepata hasara kwa maji ya mto kufunika mashamba yote.

 Hali hiyo imetokana na Bwawa la Sulungai ambalo ndiyo ukomo wa mto huo kujaa maji na kufikia kiwango chake sha mwisho hivyo, kusababisha maji yanayoletwa na Mto Bubu kufunika mashamba ya mpunga.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (mwenye kilemba chekundu) akishuka kwenye pikpiki ili kuwafikia Wakulima wa Mpunga katika Skimu ya Nguvu Mali Block namba 04 tarehe 08 Mei 2020 ambao baadhi ya mashamba yao yamefunikwa na maji yanayoletwa na Mto Bubu kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Arusha na Manyara.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (mwenye kilemba chekundu) pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo wakiangalia uharibifu wa miundombinu uliotokana na maji yaliyoletwa na Mto Bubu kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Arusha na Manyara.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (mwenye kilemba chekundu) pamoja na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo wakitumia usafiri wa mtumbwi ili kuwafikia Wakulima wa Mpunga katika Skimu ya Nguvu Mali Block namba 04 tarehe 08 Mei 2020 ambao baadhi ya mashamba yao yamejaa maji yaliyoletwa na Mto Bubu kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Arusha na Manyara. Kwa kuwa zao hilo lilisha komaa, inawalazimu kuvuna kwa kutumia mtumbwi hali ambayo inaongeza gharama kubwa kwa mkulima.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (mwenye kilemba chekundu) pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo wakimsikiliza Afisa wa Kilimo, Solomon Chapa (wa kwanza kushoto) wakati akitoa maelezo ya namna wakulima walivyopata athari na maji hayo.


Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (mwenye kilemba chekundu) akiangalia mpunga ulioanikwa ili kukausha maji baada ya kulowana na maji ya Mto Bubu yaliyofunika mashamba yao.

Mustapha Hussein ambaye ni mkulima katika Skimu ya Nguvumali block namba 04 iliyopo Kijiji cha Bahi Sokoni akishusha Mpunga wake kwenye mtumbwi na kuuanika kabla ya kuusafirisha kwenda nyumbani.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza na wakulima wa Skimu ya Bahi Sokoni na Nguvumali tarehe 08 Mei 2020.

Baadhi ya wakulima wakizungumza na kumshukuru Mkuu wa WIlaya ya Bahi (hayupo pichani) kwa uamuzi wake pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya, kuiwatembelea na wamesema kitendo hicho kimeonesha kwa Serikali inawajali na ipo karibu nao hasa katika kipindi hiki kigumu kwao.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa