• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Stakabadhi Ghalani Suluhisho 'Kangomba' Bahi

Imechapishwa: April 30th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Afisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika Wilaya ya Bahi, Awadhi Mashombo amelieleza Baraza la Madiwani kuwa Wakulima wote wa zao la Ufuta wilayani humo kuanzia mwaka huu (2020) sasa watauza zao hilo kwa Mfumo wa Stakabadhi Ghalani ili zao hilo liwe na tija kwao.

Mashombo ameyasema hayo wakati akijibu swali lililoulizwa na Diwani wa Kata ya Babayu, Hussein Kamau kwenye kikao cha Baraza la Madiwani robo ya tatu kwa mwaka wa fedha 2019/2020 aliyehitaji kujua utaratibu mpya wa kuuza zao hilo baada ya kuulizwa na wananchi wake kwa njia ya simu kwamba wanaona kuwa utaratibu umebadilika.  

Kupitia kikao hicho kilichoketi tarehe 30 Aprili 2020 kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi, Mashombo amesema kuwa mauzo ya ufuta yatasimamiwa na Chama cha Ushirika wa Kilimo na Masoko Balalu - BALALU AMCOS.

Ambapo ameeleza kwamba ufuta utakusanywa katika vituo mbalimbali vitakavyowekwa na BALALU AMCOS katika Kata na Vijiji mbalimbali. Hivyo, wafanyabiashara wote Bahi hawataruhusiwa kukusanya au kununua ufuta kwa mkulima isipokuwa kwa BALALU AMCOS ambaye ameidhinishwa na Halmashauri.

Mashombo amelieleza Baraza kuwa mfumo huo unaanza kutekelezwa baada ya kupokea maelekezo yalitotolewa na Wizara ya Kilimo, Umwagiliji na Ushirika kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara ambazo zimerasmisha zao hilo kuuzwa kwa mfumo huo.

“Kwa kuwa Wilaya yetu ina Chama cha Ushirika kimoja ambacho ni BALALU AMCOS basi kwa kushirikiana na Maafisa Ugani waliopo kwenye Kata zote, ndicho kitakachokusanya ufuta kutoka kwa wakulima na kuupeleka katika ghala ambako mnada ndiko utakakokuwa unafanyika”. Anasema Mashombo na kuongeza;

“Hivyo, ununuzi utakuwa unafanyika kwa njia ya mnada na ununuzi huo utakuwa wa ushindani kwa hiyo bei itakuwa ya mnada na siyo bei za wachuuzi ambao kila mmoja anaenda kununua kwa mkulima mmoja mmoja…wakulima watalipwa baada ya mnadakufanyika na watalipwa kupitia Benki”. Amesema Mashombo.

 Mashombo amesema kuwa ili kupambana na wakulima wasio halisi (Kangomba), tayari Halmashauri kupitia Idara hiyo imeshawapatia maelekezo Maafisa Ugani kuwatambua wakulima wote ambao wamelima zao la ufuta kwa msimu huu na siku ya kuuza atakayekuja na mzigo ndiye atakayetambuliwa.

Wajumbe wa Baraza la Madiwani wakiwa katika kikao cha tatu cha Baraza hilo kwa mwaka wa fedha 2019/2020  kilichofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi tarehe 30 Aprili 2020. 

Katibu wa Baraza la Madiwani  ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga akizungumza wakati wa kikao cha tatu cha Baraza hilo kwa mwaka wa fedha 2019/2020  kilichofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi tarehe 30 Aprili 2020. Ambapo pamoja na kuwasilishwa kwa taarifa za utekelezaji wa Jamati za Kudumu za Halmashauri pia iliwasilishwa taarifa ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa kipindi hicho.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza wakati wa kikao cha tatu cha Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2019/2020  kilichofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi tarehe 30 Aprili 2020.

Afisa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dodoma,  Nathalis Linuma akizungumza wakati wa kikao cha tatu cha Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2019/2020  kilichofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi tarehe 30 Aprili 2020.


Baadhi ya Madiwani wakizungumza wakati wa kikao cha tatu cha Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2019/2020  kilichofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi tarehe 30 Aprili 2020.

Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Bahi, Helen Mselemu akijitambulisha mbele ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani na Viongozi waliohudhuria kikao cha tatu cha Baraza hilo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 tarehe 30 Aprili 2020. Mselemu amehamia wilayani humo akitokea Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR - TAMISEMI).

Afisa Ardhi na Maliasili Wilaya ya Bahi, Utongani akijitambulisha mbele ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani na Viongozi waliohudhuria kikao cha tatu cha Baraza hilo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 tarehe 30 Aprili 2020. Utongani amehamia wilayani humo akitokea Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Baadhi ya Wataalam wakifuatilia kikao cha tatu cha Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2019/2020 kilichofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Bahi tarehe 30 Aprili 2020.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa