• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wahitimu Jeshi la Akiba Watakiwa kuwa Chachu ya Maendeleo

Imechapishwa: November 26th, 2019

Benton Nollo, Ilindi

Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi wilayani Bahi wametakiwa kuwa chachu ya Maendeleo katika jamii wanayoishi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda wakati akifunga rasmi mafunzo hayo yaliyofanyika katika Kijiji cha Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.


Munkunda amewapongeza wahitimu wote na kuwasihi kuyatumia mafunzo hayo kama chachu ya kujiletea maendeleo na kuhakikisha kuwa wanailinda jamii inayowazunguka. Aidha, amewaahidi kuwa Serikali ipo nao bega kwa bega na ndiyo maana imetumia gharama kubwa kuwapatia mafunzo hayo. Aidha, Munkunda alitumia fursa hiyo kuyaomba makampuni binafsi ya ulinzi kuwatumia vijana hao wenye mafunzo ya kijeshi kwa shughuli zao za ulinzi. 


Pia, Munkunda ametumia fursa hiyo kuwaasa vijana wilayani humo kuwa inapotokea fursa kama hiyo katika Kijiji chochote wajitokeze kwa wingi na wasikatishwe tamaa kwani Serikali inatumia gharama kubwa kufanikisha mafunzo hayo.


"Vijana wangu najua mmepitia vikwazo vingi na ninajua mlikatishwa tamaa maana wapo mabingwa wa kukatisha watu tamaa lakini mmevuka salama na leo mnahitimu, basi mafunzo haya yawe na tija katika maisha yenu binafsi na jamii inayowazunguka". Anasema Munkunda.


Mafunzo hayo ya miezi 6 yalijumuisha vijana 92 ambapo kati ya hao wanaume 84 na wanawake 8 chini ya usimamizi wa Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Bahi.


PICHA NA MATUKIO:

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akiwasili katika Uwanja wa Shule ya Msingi Ilindi kwa ajili ya kufunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akikagua Gwaride Maalum la Heshima lililoandaliwa kwa ajili yake kabla ya kufunga rasmi Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi. Hafla hiyo ilifanyika katika U wanja wa Shule ya Msingi Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

Sajenti Taji Bahati Chizenga akionesha  umahiri wa kuzuia pikipiki mbili mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bahi kwenye hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

Afisa Mteule (WO2), Bahati Muro akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Bahi (hayupo pichani) kwenye hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

MG Godliving Urio akisoma risala mbele ya Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (hayupo pichani) kwa niaba ya Wahitimu wenzie 92 wakati wa hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.  

Gwaride Maalum likipita na kutoa heshima mbele ya Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (hayupo pichani)  wakati wa hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza wakati wa hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

Baadhi ya Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi wakati wa hafla za kufunga mafunzo hayo zilizofanyika katika Kijiji cha Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akikabidhi vyeti vya pongezi katika nyanja mbalimbali kwa Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo iliyofanyika katika Kijiji cha Ilindi tarehe 26 Novemba 2019.


Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Bahi wakiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu wa Mafunzo ya Awali ya Jeshi la Akiba Kata ya Ilindi,  wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo iliyofanyika katika Kijiji cha Ilindi tarehe 26 Novemba 2019. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa