• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi, Wageni Washuhudia Dkt. Magufuli Akiapa kuwa Rais wa Tanzania

Imechapishwa: November 5th, 2020

Rais Mteule Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameapishwa rasmi leo tarehe 05 Novemba 2020 jijini Dodoma huku akishuhudiwa na maelfu ya wananchi wa Watanzania pamoja na wageni waalikwa kutoka mataifa mbalimbali wakiwemo Marais, Makamu wa Rais , Mawaziri na viongozi wa dini.

Kabla ya kula kiapo, Dky. Magufuli aliingia Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma majira ya saa nne asubuhi na kisha kuzunguka uwanja kwa ajili ya kuwasalimia wananchi walijitokeza kushuhudia tukio hilo akiwa katika gari ya wazi.

Baada ya kuzunguka uwanja alishuka kwenye gari na kisha kuelekea eneo maalum kwa ajili ya Wimbo wa Taifa pamoja na mizinga 21. Baada ya hapo ikashushwa bendera ya Rais ikiwa ni ishara ya kuhitimisha Muhula wa Kwanza wa uongozi wake katika kipindi cha Awamu ya Tano.

Hata hivyo, baada ya kushushwa Bendera ya Rais, Dkt. Magufuli alielekea kwenye jukwaa maalum kwa ajili ya kula kiapo ambapo Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma ndiye aliyemuapisha na kisha alipewa ngao na wazee wawili mmoja kutoka Tanzania Bara na mmoja kutoka Tanzania Visiwani.

Dkt. Magufuli baada ya hapo alikaa kitini na kisha ikafuata hatua ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kula kiapo cha kutumikia nafasi hiyo. Walipomaliza kula kiapo ikafuata nafasi ya dua ambayo iliombwa na viongozi wa dini zote.

Baada ya dua hiyo kumalizika Rais Dkt. Magufuli, Makamu wa Rais wakiwa wameongozana na Jaji Mkuu, wazee, viongozi wa dini, Mwanasheria Mkuu wa Serikali walifanya maandamano kutoka kwenye jukwaaa ambalo lilitumika kwa ajili ya kumuapisha huku gwaride maalum likiwa limetengeneza umbo la Alfa ikiwa ni ishara ya kuanza kwa muhula wa pili wa miaka mitano ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Wakati tukio hilo likiendelea utulivu uwanjani hapo ulikuwa mkubwa, wananchi na wageni waalikwa walikuwa kimya, Rais Dkt. Magufuli alienda eneo maalum kwa ajili ya gwaride hilo lilikuwa katika umbo la Alfa na baadaye mizinga mingine 21 ilipigwa. Baada ya hapo alikagua gwaride hilo huku ndege za kivita zikipita angani.

Rais Dkt. Magufuli baada ya kumaliza kukagua gwaride alienda moja kwa moja jukwaa kuu. Wakati huo wananchi na wageni waalikwa wote walikuwa wamesimama huku shangwe zikirindima. Gwaride liliendelea kutoa burudani na kisha kufuatiwa tena na Wimbo wa Taifa.

Hata hivyo, gwaride maalum ambalo liligawanyika katika sehemu tatu ikiwemo kikosi cha Askari waliobeba Bendera ya Rais. Hata hivyo gwaride likipita mbele ya Rais shangwe zilitawala uwanjani hapo hasa walipoingia makomandoo.

Baada ya gwaride kutoka uwanjani ilifuata hatua ya utambulisho wa wageni waliohudhuria tukio hilo la kihistoria ambalo hutokea kila baada ya miaka mitano. Baadhi ya wageni hao ni Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museven, Rais wa Comorro, Kazar Othaman na Rais wa Zimbabwe Emmason Mnangagwa. Pia, wametambulishwa wawakilishi wa nchi mbalimbali pamoja na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini Tanzania.

MATUKIO KATIKA PICHA:

Rais Mteule Dkt. John Pombe Joseph Magufuli (anayepunga mkono juu ya gari) akiwasalimia maelfu ya wananchi na wageni mbalimbali waliojitokeza kushuhudia kiapo chake kwa ajili ya kuiongoza Tanzania muhula wa pili wa Serikali ya Awamu ya Tano. Sherehe hizo zimefanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma  leo tarehe 05 Novemba 2020.

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John  Pombe Magufuli  akielekea katika jukwaa baada ya kuapishwa tarehe 5 Novemba 2020 katika Uwanja wa Jamuhuri jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuapishwa tarehe 05 Novemba 2020 katika sherehe zilizofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Wananchi na Wageni mbalimbali wakifuatilia shughuli za sherehe za Uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 05 Novemba 2020 zilizofanyika katika Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. (Picha zote na Ikulu).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa