• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wapangaji Kituo cha Ufundi Kigwe Watakiwa Kutunza Mazingira

Imechapishwa: April 2nd, 2020

Na Benton Nollo, Kigwe

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amewataka Wapangaji wa majengo ya kilichokuwa Kituo cha Ufundi wa Zana za Kilimo kutunza mazingira, wakati huu ambapo Serikali inajipanga kufufua chuo hicho kilichopo Kijiji cha Mapinduzi Kata ya Kigwe wilayani humo.

Munkunda ameyasema hayo baada ya kufanya ukaguzi wa majengo 16 na miundombinu mbalimbali iliyopo kituoni hapo tarehe 02 Aprili 2020.

“Ndugu zangu Wapangaji nimesikitishwa sana kulikuta eneo hili likiwa katika hali ya uchafu uliokithiri ilhali ninyi mpo na kwa baadhi ya majengo wenzenu wengine wanadiriki kuweka mifugo jambo ambali linahatarisha usalama wa majengo haya ambayo ni muhimu kwa matumizi ya baadaye”. Anasema Munkunda na kuongeza,

“Eneo hili lina mali nyingi na ni muhimu sana kwa kukuza uchumi wa Wilaya yetu ya Bahi hivyo, linatakiwa kuwa safi wakati wote”.

Kutokana na changamoto ya wapangaji hao kutolipa Kodi ya Pango kwa wakati na wengine kutolipa kabisa, Munkunda  ametoa siku 30 ambapo kuanzia tarehe 01 Mei 2020 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ambayo ndiyo mmiliki wa Kituo hicho itapanga utaratibu mpya wa namna ya kulipa Kodi ya Pango na matumizi ya eneo hilo.

Pia, Munkunda ameuagiza uongozi wa Kijiji cha Mapinduzi na Kijiji cha Kigwe kuhakikisha kuwa mpaka tarehe 30 Aprili 2020 mabati na baadhi ya vifaa vilivyoibiwa kituoni hapo viwe vimepatikana.

Kituo hiki kilijengwa kwa kibali cha Mkurugenzi wa Maendeleo Mkoa wa Dodoma - RDD mwaka 1975 na kilianza kufanya kazi rasmi mwaka 1976 kikisimamiwa na Wizara ya Kilimo na maelekezo ya uendeshaji yalikuwa yakitolewa na Taasisi ya Majaribio ya Zana za Kilimo Arusha - TAMTU (Tanzania Agricultural Machinery Testing Unit).

Mwaka 1980 Shirika la Kijerumani la KUBEL STIFTANG kupitia Mradi wa Maendeleo Mkoa wa Dodoma – DODEP lilianza kutoa ruzuku na kupanua chuo hicho kwa kuongeza nyumba za watumishi.

Aidha, ilipofika mwaka 1996 Kituo kilikabidhiwa kwa Halmashauri ya WIlaya ya Dodoma Vijijini wakati huo ambayo kwa sasa ni Bahi na kwa kuwa Halmashauri hiyo haikuwa na uwezo wa kukiendesha kituo hicho tarehe 04 Desemba 2003 ilikikabidhi kwa mkataba Kituo kwa Shirika la KISEDET (Kigwe Social Economic Development and Trainning).

 Ambapo ilipofika tarehe 10 Agosti 2016, shirika la KISEDET liliamua kurudisha Kituo hicho kwa Mmiliki wake ambaye ni Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Majengo yaliyokabidhiwa ni nyumba 16, bweni 1, madarasa 6, jengo 1 la utawala lenye ofisi 5, mabanda ya mifugo 2, mtambo wa Biogas na jengo la karakana.

PICHA NA MATUKIO:

Baadhi ya Majengo ya Kituo cha Ufundi Kigwe yakiwa katika hali ya uchafu.

Pichani juu ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akikagua majengo na zana zilizopo katika Kituo cha Ufundi Kigwe tarehe 02 Aprili 2020 ambapo pia aliambata na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo.

Mkuu wa Wilaya na Bahi, Mwanahamisi Munkunda (mwenye kiremba cha bluu) akiwa katika kikao cha pamoja na wapangaji wa Kituo cha Ufundi Kigwe ambapo pia kilihudhuriwa na wajumbe wa Serikali za Vijiji vya Kigwe na Mapinduzi tarehe 02 Aprili 2020. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa