• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wataalam wa Afya Watakiwa Kusimamia Ukarabati Vituo vya Afya

Imechapishwa: October 9th, 2018

Na Benton Nollo

Wataalam na Wadau wa afya mkoani Dodoma wametakiwa kusimamia vema ukarabati wa Vituo vya Afya unaoendelea hivi sasa mkoani humo ili vituo hivyo wiweze kuanza kutoa huduma za uzazi na mtoto mapema. Hayo yamesemwa na Katibu Tawala Wilaya ya Bahi, Jeremia Mapogo aliyekuwa Mgeni Rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo kwenye ufunguzi  wa kikao cha siku mbili kinachofanyika kimkoa wilayani humo kujadili vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga kwa kipindi cha Aprili hadi Juni, 2018.

Mapogo alifafanua kuwa uboreshaji wa vituo hivyo kwa kiasi kikubwa utafanya lengo la mkoa wa Dodoma kupunguza vifo hivyo kutoka 60/100,000 mpaka 55/100,000 ya vizazi hai ifikapo Desemba, 2018 ambapo kwa sasa kiwango cha vifo Kimkoa ni 60/100,000 ya vizazi hai hali ambayo takwimu hizi inaonyesha kuwa bado kuna kazi kubwa ya kufanya kama mkoa ili kuweza kufikia malengo yaliyopangwa.

Aidha, Mapogo alieleza kuwa pamoja na mikakati ambayo Wataalam hao wamejiwekea, pia anatambua kuwa kuna changamoto nyingi zinazozuia kufikia malengo ya kupunguza vifo hivyo ambayo alizitaja kuwa ni; Mwitikio hafifu kutoka kwa wananchi, yaani (akina mama kutozalia katika vituo vya huduma za afya), pamoja na kuchelewa kuanza kliniki chini ya umri wa miezi mitatu (3), Vituo vichache vya kutolea huduma za afya kwani bado hatujafikia lengo la serikali la kila kijiji kuwa na Zahanati na kila Kata kuwa na Kituo cha Afya, Matumizi madogo ya njia za uzazi wa mpango katika jamii, Upungufu wa wataalamu wa afya kuendana na Ikama, Upungufu wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya huduma za afya, Upungufu wa magari ya kubebea wagonjwa hususani wagonjwa wa dharura kama wajawazito,Mwitikio hafifu wa elimu ya uzazi na mtoto inayotolewa kwa jamii nzima na changamoto nyinginezo kwa kila Wilaya.

Mapogo aliwapongeza wataalam hao kuwa pamoja na changamoto hizo lakini bado wameonesha mikakati ambayo wamejiwekea katika kutekeleza azma ya serikali ya awamu ya tano ya kupunguza vifo vya akinamama vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga mkoani Dodoma kwa kuhakikisha wajawazito na wenza wao wanahudhuria kliniki mara mama apatapo ujauzito, kuongeza kiwango cha kujifungulia katika vituo vya huduma za afya kutoka asilimia 81 hadi asilimia 85 ifikapo Desemba, 2018.

Pia, kuongeza mahudhurio ya kliniki kwa wazazi baada ya kujifungua kutoka asilimia 48 hadi asilimia 80 ifikapo Desemba, 2018, kuendelea kuboresha huduma za chanjo kufikia kiwango cha  asilimia 95 kwa watoto ifikapo Desemba, 2018, kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na CHF iliyoboreshwa, kuhakikisha Hospitali zote 8 zilizopo katika Mkoa wa Dodoma zinatoa huduma ya njia ya kangaroo kwa watoto wanaozaliwa njiti ifikapo Desemba, 2018 na kuhakikisha vituo vya afya 8 kati ya  36 vinatoa huduma ya dharura ya upasuaji kwa akina mama wajawazito ifikapo Desemba, 2018.

Kadhalika, Mapogo alieleza kuguswa na kuhamasika na mikakati iliyowekwa ili kutekeleza lengo la kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga, na kwa upande wa serikali aliahidi kusimamia utekelezaji wa mikakati hiyo.

"Ndugu zangu Wataalam napenda kuwatia moyo muendelea kupambana na changamoto nilizozitajwa awali na nyinginezo, ili tuweze kufikia malengo tuliyojiwekea na kuinua kiwango cha huduma za afya katika nyanja zote, kwa Mkoa wetu wa Dodoma". Alisema Mapogo na kuongeza kuwa

"Kama mlivyojiwekea taratibu za vikao hivi vya kujadili vifo vya  akina mama vitokanavyo na uzazi na watoto wachanga kila robo mwaka kwa kupokezana kila wilaya, endeleeni hivyo hivyo kwani vikao hivi vinatoa picha halisi ya hali ilivyo katika mkoa wetu na kutusaidia kujitathimini kama mkoa na kwa sababu mkoa wetu tuna mikakati mizuri ya kupunguza vifo hivyo, basi  tutarajie wageni wengi kuja kujifunza kwetu ili na wenyewe waweze kufaidika kutoka kwetu".

Aidha, akizungumza wakati akimkaribisha mgeni rasmi, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Mzee Nassoro alisema kuwa kikao hicho kinahusisha wadau katika sekta ya afya na wataalam wa afya kutoka ngazi ya mkoa na wilaya zote saba (7) za mkoa wa Dodoma. 


Kwa picha na matukio tazama hapo chini:

Mganga Mkuu Wilaya ya Bahi, Dkt. Philipina Philipo akizungumza wakati wa Mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi tarehe 09 Oktoba, 2018. (Picha na Benton Nollo)

Kaimu Mganga Mkuu Mkoa wa Dodoma, Dkt. Mzee Nassoro akizungumza wakati wa Mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi tarehe 09 Oktoba, 2018. (Picha na Benton Nollo)

Wataalamu na Wadau wa Sekta ya Afya wakifuatilia moja ya mawasilisho katika mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi tarehe 09 Oktoba, 2018. (Picha na Benton Nollo)

Wataalamu na Wadau wa Sekta ya Afya wakifuatilia moja ya mawasilisho katika mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi tarehe 09 Oktoba, 2018. (Picha na Benton Nollo)

Wataalamu na Wadau wa Sekta ya Afya wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi (wa pili kushoto waliokaa) mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi tarehe 09 Oktoba, 2018. (Picha na Benton Nollo)

Wataalamu na Wadau wa Sekta ya Afya wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi (wa pili kushoto waliokaa) mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi tarehe 09 Oktoba, 2018. (Picha na Benton Nollo).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • NOTISI YA KUVUNJWA KWA MABARAZA YA MADIWANI KATIKA MAMLAKA ZA WILAYA NA MIJI YATOLEWA NA MHE.MCHENGERWA

    June 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI YATWAA TUZO YA UBINGWA

    June 15, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI NA KUWA WABUNIFU

    May 23, 2025
  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa