• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Bahi Yatoa Tuzo za Umahiri kwa Walimu

Imechapishwa: February 17th, 2021

Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi

Halmashauri ya Wilaya ya Bahi imewazawadia walimu mahiri fedha, kompyuta na mavazi katika masomo mbalimbali pamoja na shule kumi bora katika mtihani wa Darasa la Saba na Kidato cha Nne ili kutoa motisha kwao kwani kwa matokeo ya Darasa la Saba 2020 Wilaya ya Bahi imekuwa ya kwanza kwa Mkoa wa Dodoma.

Pamoja na zawadi hizo pia, Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kwa shule kumi duni mwaka 2020 imetoa bendera nyeusi ili ziwakumbushe kwamba wanapaswa kujituma na kuimarisha elimu katika shule zao.

Zawadi hizo zimetolewa kupitia kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021 katika uwanja wa Jengo la Makao Makuu ya Halmashauri na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa elimu.

Akizungumza baada ya kukabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Jeremia Mapogo amewaasa walimu kufanya kazi kwa uadilifu kwani taifa linawategemea sana na kusema kuwa  kazi yao niya  kipekee kwa kuwa hakuna mtaalamu yeyote ambaye hakupitia mikono ya Mwalimu.

“Mzazi anamzaa mtoto anamlea kwa hatua fulani anamlisha na kuendelea kumpa mahitaji yote, lakini Mwalimu anakuwa na mtoto katika umri wake wote wa kujifunza na anamuandaa tayari kwenda kupambana na maisha yanayotuzunguka hivyo kazi yenu ni nyeti sana.” Amesema Mapogo.

Naye Mbunge wa jimbo la Bahi Kenneth Nollo (Mb) akizungumza katika kikao hicho amesema hatamfumbia macho mtu yeyote atakayeshiriki kumpa ujauzito msichana wa shule na kuahidi kupambana kwa uwezo wake wote kutokomeza tatizo hilo.

Akizungumza na walimu katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga amewaonya walimu kujiepusha na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi badala yake wazingatie maadili ya kazi yao ili wawe na ufanisi katika kazi zitakazoiwezesha halmashauri kuendelea kulinda kiwango cha elimu walichokifikia kwa sasa.

Awali, akitoa taarifa kuhusiana na tuzo hizo, Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Bahi, Boniface William amesema zawadi zilizotolewa zimehusisha Walimu mahiri katika masomo mbalimbali kwa shule za Msingi na Sekondari yakiwemo masomo ya Hisabati, Sayansi, Fizikia, Siasa, Kemia  na masomo mengine pamoja na kuzawadia shule kumi bora na kumi duni kwa shule za msingi na sekondari  katika matokeo kwa mwaka wa masomo 2020.


Picha na Matukio:

Picha zote juu ni zawadi kwa shule na walimu wa masomo waliofanya vizuri kwenye mitihani ya taifa ya mwaka 2020 shule za msingi na sekondari wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021..

Picha zote za juu ni walimu wa shule  zilizofanya vibaya kwenye mitihani ya taifa ya mwaka 2020 shule za msingi na sekondari wakipokea bendera nyeusi wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari, 2021.

Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Bahi, Boniphace William akiwasilisha taarifa ya elimu msingi na sekondari kwa mwaka 2020 wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Mthibiti Ubora wa Shule Wilaya ya Bahi, Pudenciana Kuzenza akiwasilisha tathmini ya ubora wa shule za msingi wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Donald Mejiti akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Pius Mwaluko akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo (Mb) akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Picha zote za juu ni viongozi na wadau wa elimu wakitoa mawazo yao juu ya namna ya kuboresha sekta ya elimu ili kukuza ufauli wilayani Bahi wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Baadhi ya Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu wakitoa uzoefu kwa namna walivyofanikisha kuongeza ufaulu katika mitihani ya taifa ya mwaka 2020 wakati wa kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Bahi kilichofanyika tarehe 17 Februari 2021.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa