• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chisomi: Walipeni Vibarua kwa Wakati kukamilisha Miradi ya Afya na Maji

Imechapishwa: June 26th, 2018

Na Benton Nollo, Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Mhe. Danford Chisomi amewataka Mafundi na Mkandarasi walioshinda zabuni ya ujenzi wa majengo matano katika Zahanati ya Chifutuka na ile ya Utafiti na Uchimbaji wa Kisima cha maji Kijiji cha Nghulugano, kuwalipa vibarua wao kwa wakati na kuwasimamia wakati wote ili miradi hiyo ikamilike kwa ubora na kwa muda uliopangwa kwenye mkataba. Chisomi ameyasema hayo Juni 26, 2018 mara baada ya kusaini mikataba baina ya Halmashauri ya Wilaya ya Bahi na Mafundi watakaojenga majengo matano kwa mfumo wa "Force Account" katika Zahanati ya Chifutuka pamoja na Utafiti na Uchimbaji wa Kisima cha maji Kijiji cha Nghulugano.

"Serikali Kuu tayari imeshatuingizia fedha shilingi 500,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika Zahanati ya Chifutuka, hivyo sisi kama Halmashauri kupitia Ofisi ya Mweka Hazina wa Wilaya tutahakikisha mafundi wote wanalipwa kwa wakati na vifaa vinanunuliwa na kupelekwa eneo la mradi haraka ili ndani ya siku 90 majengo yote yawe yamekamilika". Alisema Chisomi na kuongeza kwa kumkumbusha Mweka Hazina kuwakata mafundi hao Kodi ya Zuio ambayo ni asilimia 5 kwa kila malipo watakayohitaji.   

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Rachel Chuwa amewataka mafundi hao kusoma vizuri vipengele vyote vya mikataba yao ili waelewe na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. 

"Ni wajibu wa kila fundi kusoma kwa makini na kuyaelewa vema majukumu anayopaswa kutekeleza kwani ni matarajio ya wananchi kuona miradi hiyo inakamilika kwa wakati ili waweze kupata huduma kama ilivyokusudiwa na Serikali. Pia, kila fundi ahakikishe kuwa anawasimamia vibarua wake ili kuepuka upotevu wa vifaa hali ambayo itadhoofisha utekelezaji wa mradi". Alisema Chuwa.    

Akizungumza kwa niaba ya mafundi wenzake, Nassoro Twaibu Nambinga atakayejenga nyumba ya mtumishi Zahanati ya Chifutuka ameiomba Halmashauri kununua vifaa na kuvipeleka eneo la mradi kwa wakati ili kusiwe na ucheleweshaji wa kazi kwa kisingizio cha vifaa kuchelewa.   

Ujenzi wa majengo Zahanati ya Chifutuka unajumuisha jengo la upasuaji ambapo fundi ni Robert N. Makapi na gharama ya ufundi ni shilingi 21,280,000.00, jengo la Wodi ya Akinamama na Watoto fundi ni Hassan R. Mvungi gharama za ufundi ni shilingi 22,750,000.00 na ujenzi wa Jengo la Maabara Fundi ni Sembisa Alfredy  gharama ya ufundi ni shilingi 16,600,000.00. Majengo mengine ni Nyumba ya Mtumishi  fundi ni Nassoro Nambinga atakayejenga kwa shilingi 14,100,000.00, jengo la Kuhifadhia Maiti fundi ni Hosea L. Shansi kwa gharama ya shilingi 12,500,000.00. 

kwa upande wa mradi wa Utafiti na Uchimbaji wa Kisima katika Kijiji cha Nghulugano utakaotekelezwa na Mkandarasi Target Borewells Ltd kwa gharama ya shilingi 30,680,000.00 na mradi utatekeleza kwa muda wa siku 15 kuanzia Juni 26, 2018.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa