• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Munkunda: Madiwani Shirikianeni Kutatua Kero za Wananchi

Imechapishwa: December 14th, 2020

Na Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi 

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda ametoa rai kwa  Madiwani  wa wilaya hiyo kuhakikisha kuwa katika uongozi wao wanashirikiana na viongozi wa Kata na Vijiji  ili  kutatua kero zinazowakabili  wananchi.

Munkunda ametoa rai hiyo wakati wa uzinduzi wa Baraza Jipya la Madiwani katika Mkutano wa Kwanza uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi tarehe 14 Desemba 2020 kwa ajili ya kuwaapisha Madiwani hao, kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti  wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi.

Amesema Madiwani wahakikishe wanayasimamia vema Mabaraza ya Kata katika maeneo yao kwani ndiko chimbuko la maendeleo lilipo ikiwa ni pamoja na kuyaimarisha na kuyasimamia vema mabaraza ya ardhi ya kata ili kutatua migogoro mingi ya ardhi iliyopo katika maeneo yao.

“Kiongozi lazima ujue kuwa upo kwa ajili ya kutatua matatizo ya wananchi, shirikianeni na viongozi wa vijiji na kata kutatua changamoto zinazowakabili wananchi kwani wamewaamini ndiyo maana wamewachagua hivyo, hakikisheni mnawatumikia ipasavyo.” Amesema Munkunda.

Mkuu huyo wa Wilaya pia, amewaagiza Madiwani hao kuhakikisha maeneo yote ya wazi ambayo ni mali ya kijiji yanarudi Serikalini ili yaweze kusimamiwa na kupangiwa matumizi kwa manufaa ya Wananchi wote badala ya kuhodhiwa na watu wachache.

“Hakikisheni maeneo yote ambayo ni mali ya Kijiji yanarudi Serikalini, pia ni marufuku watu kupiga uzio maeneo ya wazi na kujimilikisha jambo hilo haliwezekani, ni lazima Serikali tuwe na benki ya ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya maendeleo.” Amesema Munkunda.

Awali akifungua Mkutano wa Kwanza wa Baraza Jipya la Madiwani Mwenyekiti ambaye pia ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Bahi, Jeremia Mapogo amewataka Madiwani kuwa na mshikamano ili waweze kupata ufanisi  kwenye majukumu waliyopewa.

“Niwapongeze Madiwani wote kwa kuchaguliwa kuwa wawakilishi wa Wananchi, kazi mliyopewa ni nyeti, hakikisheni mnakuwa na mshikamano katika kazi zenu ili muwe na ufanisi.” Amesema Mapogo na kuongeza;

“Mnao wajibu wa kuleta maoni ya wananchi Halmashauri na kurudisha mrejesho kwao ili kwa pamoja tuyasukume maendeleo mbele.”

Akizungumza baada ya kuchaguliwa kuwa Menyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kwa kipindi cha miaka mitano (2020 – 2025), Donald Simango Mejiti ambaye ni Diwani wa Kata ya Lamaiti  amewashukuru Madiwani kwa kuonesha imani kwake na kuomba ushirikiano ili kwa pamoja waweze kuleta maendeleo kwa Wananchi.

“Niwashukuru sana kwa kuonyesha imani kwangu, niombe ushirikiano wenu kwani kamwe hatuwezi kuiendesha Halmashauri bila kuwa na ushirikiano, tuwe na uzalendo na mshikamano ili tuongeze tija katika maendeleo ya wilaya yetu.” Amesema Mejiti.

Katika Uchaguzi huo, Mejiti alichaguliwa kwa kura za NDIYO 29 kati ya kura 30 zilizopigwa sawa na asilimia 96.7, naye Diwani wa Kata ya Chali, Pius Donald Mwaluko amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kura za NDIYO 28 kati ya kura 30 zilizopigwa sawa na asilimia 93.3.

Pamoja na uchaguzi huo pia ulifanyika uchaguzi wa wajumbe wa Kamati za Kudumu za Halmashauri ambapo Diwani wa Kata ya Mpamantwa, Sosthenes Mpandu alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji (EAM) ambapo Diwani wa Kata ya Msisi, Mathayo Malilo alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira (UUM).

Baraza hilo limeketi kwa mara ya kwanza baada ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020, ambapo tangu kuanzishwa kwa Halmashauri hiyo mwaka 2007 hili ni Baraza la Tatu.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza kwenye kikao hicho.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ambaye pia ni Katibu wa Mkutano wa Kwanza wa Madiwani, Dkt. Fatuma Mganga akiwakaribisha Madiwani kwenye mkutano huo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Donald Mejiti akiendesha kikao cha Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Madiwani mara baada ya kuchaguliwa.

Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo, (Mb) akizungumza wakati wa kikao cha Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Madiwani.

Afisa Mipango wa Wilaya ya Bahi, Charles Mduma akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri katika kipindi ambacho Madiwani hawakuwepo.

Viongozi meza kuu wakifuatilia kwa makini taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Halmashauri katika kipindi ambacho Madiwani hawakuwepo iliyokuwa ikiwasiilshwa na Afisa Mipango wa Wilaya ya Bahi, Charles Mduma (hayupo pichani).

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Pius Donald Mwaluko akiwashukuru Madiwani baada ya kumchagua kushika wadhifa huo kwa kipindi cha mwaka mmoja (2020/2021).

Baadhi ya Waheshimiwa Madiwani wakila Kiapo cha Uadilifu mara baada ya kula kiapo cha udiwani.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa