• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC Bahi, Mkakati wa Kupunguza "Ziro" Shule za Sekondari

Imechapishwa: August 28th, 2018

Na Benton Nollo

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amewataka viongozi wa Vijiji, Kata na Tarafa zote katika Wilaya ya Bahi kuhakikisha kuwa wanawahamasisha wananchi kuchangia chakula kwa ajili ya wanafunzi hasa wa Kidato cha Nne ili waweze kujiandaa vema na mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2018. Munkunda ameyasema hayo katika Kijiji cha Mtitaa alipokuwa akizungumza na viongozi wa Tarafa ya Mtitaa  wakati wa ziara yake ya kujitambulisha tarehe 28 Agosti, 2018.

Munkunda aliwaeleza viongozi hao kuwa ili Wilaya ya Bahi isonge mbele kimaendeleo suala la elimu linatakiwa kuwekewa mkazo na mkakati madhubuti kwani kwa kufanya hivyo sekta nyingine zote zitaboreka kwa kuwa vijana watakuwa wamejikwamua kielimu.

"Ndugu zangu ili Wilaya ya Bahi isonge mbele, sekta ya elimu ni eneo muhimu sana la kulitazama na kuliendeleza kwa kuliwekea mkakati madhubuti. Wazazi wahamasishwe kuandaa Kambi za wanafunzi  kujisomea ili kuongeza ufaulu na kupunguza ziro katika Shule zetu za Sekondari". Alisema Munkunda na kuongeza kuwa,

"Mimi kama kiongozi wenu ningependa kufahamu mkakati wenu katika kuboresha na kukuza sekta ya elimu katika wilaya yetu kwamba nyinyi kama viongozi mmejipa vipi, mmejipanga kuongeza ziro au mmejipanga kupunguza ziro? Na mipango yenu ni ipi? Watoto wameanza makambi kama watoto wameanza makambi au kama hawajaanza mmeshawahamasisha kwa kiasi gani ili waanze hayo makambi na je wazazi nao wameshahamasishwa kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao? Hivyo, nategemea kupata hizo taarifa ili nipate kujua hali halisi ya shule za Sekondari zilizopo Tarafa ya Mtitaa".    

Picha Namba 1

Picha Namba 2

Picha namba 1 na 2 hapo juu ni baadhi ya viongozi wa Tarafa ya Mtitaa wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (hayupo kwenye picha zote) aliyekuwa akizungumza nao kwenye kikao cha ndani kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Kituo cha Kilimo Mtitaa tarehe 28 Agosti, 2018.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Rachel Chuwa ambaye aliambatana na kiongozi huyo, alisema kuwa dhana ya elimu bila malipo haimaanishi wazazi wasishiriki mipango ya kuinua kiwango cha elimu kwa watoto wao hivyo uongozi wa vijiji uhamasishe kuhakikisha kuwa shule zinakuwa na chakula kwa ajili ya wanafunzi wanapata huduma ya chakula wawapo shuleni ili kurahisisha maandalizi ya wanafunzi kujiandaa katika masomo yao.

Pia, aliwahimiza viongozi hao kusimamia suala la wananchi kujiunga na CHF Iliyoboreshwa ambayo kwa sasa ni shilingi 30,000.00 kwa watu sita (6) badala ya shilingi 10,000.00 kwani huduma za afya zimeongezwa. Kadhalika, aliwakumbusha viongozi kuwahimiza wananchi kujenga vyoo bora na kuvitumia ili kujikinga na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.   

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Rachel Chuwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na viongozi wa Tarafa ya Mtitaa tarehe 28 Agosti, 2018

Aidha, pamoja na suala la elimu, DC Munkunda alisisitiza suala la Watendaji wa Vijiji na Kata kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kuzuia mianya ya upotevu wake, kuwahamasisha wananchi kutambua fursa za uwekezaji zilizopo katika maeneo yao ili wawekeze kwa lengo la kujikwamua na umaskini na kukuza uchumi katika familia zao na kwa kufanya hivyo uchumi kwa Wilaya ya Bahi utakuwa. 



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa