• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Dkt. Mganga: Jiepusheni Ulevi, Mjikinge na Corona

Imechapishwa: April 30th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Afisa Mwandikishaji Jimbo la Bahi, Dkt. Fatuma Mganga amewaagiza BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi kujiepusha na ulevi ili zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili lisiwe na dosari yoyote.

Dkt. Mganga ameyasema hayo tarehe 30 Aprili 2020 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Bahi, wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi 45 waliochaguliwa kwa ajili ya zoezi hilo litakalofanyika katika Kata 22 za wilaya hiyo kuanzia tarehe 02 hadi tarehe 04 Mei, 2020. 

“Twende kule tukajiheshimu tuwe na maadili ya hali ya juu, hata kama wewe ni mlevi yaani kwa siku hizi ngapi hakikisha kwamba hujihusishi na ulevi ili uweze kufanya kazi ya watu vizuri”. Anasema Munkunda.

Aidha, pamoja na tahadhali hiyo Dkt. Mganga amewakumbusha BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi kuchukua tahadhali dhidi ya ugonjwa wa Covid 19 unaosababishwa na Virusi vya Corona katika kipindi chote cha uboreshaji wa Daftari hilo.

Dkt. Mganga amesema kuwa kutokana na ugonjwa huo zipo nchi duniani zimezuia watu wake kutoka nje na kwa kufanya hivyo nchi hizo zimeathirika sana kiuchumi kwani shughuli za uzalishaji mali zimesimama.

“Lakini kwa maono mapana ya Rais wetu, ameona ni vema sisi tukaendelea na michakato ya shughuli zetu kwa kuchukua tahadhali, maanaake tunafahamu ugonjwa unaambukizwaje, tukichukua tahadhali na huku tunaendelea kufanya kazi, hatutayumbisha uchumi wa nchi yetu”. Anasema Dkt. Mganga na kuongeza;

“Michakato mingi ambayo inatakiwa kufanyika itaendelea kama kawaida na hasa tukizingatia mwaka huu ndiyo mwaka wa uchaguzi…ni lazima tuchukue tahadhali za kujikinga sisi wenyewe na wateja wetu watakaokuja kuboresha taarifa zao.

Dkt. Mganga amewasisitiza BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi kujikinga na ugonjwa huo kwa kuvaa Barakoa wakati wote wawapo vituoni mwao na kuwaelekeza wananchi wanaokwenda kuboresha taarifa zao kunawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni na kupaka vitakasa mikono ambapo vifaa vyote hivyo alisema vimetolewa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika vituo vyote 22 ili kuwakinga na kuwalinda wananchi dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona katika kipindi chote cha zoezi hilo.

 “Watu wasisonamane kituoni, toeni maelekezo ya watu kukaa mbalimbali na hakikisha kila wakati kwenye kituo chako kuna maji na sabuni…maji yakiisha zoezi lisiendelee mpaka maji yamepatikana na hata wakati wa kuelekezana msikalibiane na muwaelimishe wananchi kwa upendo ili watambue na kuelewa umuhimu wa kunawa mikono na isionekane kuwa kwa wao kunawa mikono wananyanyapaliwa”. Anasema Dkt. Mganga.

Baadhi ya Washiriki katika Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili (BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi) wakisikiliza kwa makini hotuba ya ufunguzi iliyokuwa ikitolewa na Afisa Mwandikishaji  Jimbo la Bahi, Dkt. Fatuma Mganga (hayupo pichani) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri tarehe 30 Aprili 2020.

Baadhi ya Washiriki katika Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili (BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi) wakiapa kiapo cha utii kwenye mara baada ya Hotuba ya Ufunguzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri tarehe 30 Aprili 2020.

Wasimamizi Wasaidizi Ngazi ya Wilaya wakitoa maelekezo na ufafanuzi kwa Washiriki wa Mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Awamu ya Pili (BVR Kit Operators na Waandishi Wasaidizi) kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri  ya Wilaya ya Bahi tarehe 30 Aprili 2020. Zoezi hilo la siku tatu linafanyika kuanzia terehe 02 hadi tarehe 04 Mei 2020 katika Kata zote 22 za wilaya hiyo.   

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa