• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Jafo: Marufuku Wanafunzi Kuzuiliwa Kuandikishwa

Imechapishwa: January 7th, 2020

Na Benton Nollo, Bahi

Walimu nchini zimetakiwa kutowazuia wanafunzi kuandikishwa Darasa la Kwanza kwa mwaka wa masomo wa 2020 kwa sababu ya kukosa Cheti cha Kuzaliwa.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), wakati wa ziara yake Wilayani Bahi kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika shule za sekondari tarehe 07 Januari 2020.

Jafo amesema ni marufuku mwanafunzi kuzuiliwa kuandikishwa Darasa la Kwanza kwa sababu ya kukosa Cheti cha Kuzaliwa.

Amesema amepokea malalamiko kutoka katika baadhi ya maeneo nchini kuwa wanafunzi wa Darasa la Kwanza hawaandikishwi kama hawana vyeti vya kuzaliwa.

“Nimeona nitoe ufafanuzi kuhusu suala hili kuwa cheti cha kuzaliwa ni haki ya kila mtoto lakini isimzuie mtoto huyo kuanza shule eti kwa sababu tu hajapata cheti hicho; Watoto wote wapokelewe, waandikishwe na waanze masomo huku wazazi wao wakiendelea na mchakato wa kuwatafutia vyeti hivyo”. Amesema Jafo na kuongeza.

“Sitaki kusikia eneo lolote nchini mtoto ameachwa kupokelewa kuanza shule kwa sababu ya kukosa cheti cha kuzaliwa, mzazi ahakikishe ndani ya miezi minne amepata cheti hicho lakini mtoto huyo aanze masomo mara moja wakati masuala ya cheti yanaendea kushughulikiwa na mzazi kwenye mamlaka husika”.

Akizungumza wakati akikagua mapokezi ya Kidato cha Kwanza katika Shule ya Sekondari Bahi Wilayani humo amesema wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika muda uliopangwa na wapokelewe bila masharti ya kuleta dawati, unga, mahindi au maharage.

Ambapo aliongeza kuwa Walimu watambue Serikali inatoa Elimumsingi bila malipo hivyo, kila mwanafunzi anatakiwa kupata elimu bila bughudha yoyote.

Waziri Jafo amepongeza uongozi wa Wilaya ya Bahi kwa umakini waliouonyesha katika zoezi zima za uandikishaji wa Darasa la Kwanza linaloendelea na maandalizi mazuri ya kuwapokea wanafunzi wa Kidato cha Kwanza, na hata katika usimamizi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya hiyo hasa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Bahi mjini na Vituo vya Afya vitatu vya Bahi, Mundemu na Chifutuka.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda amesema katika Halmashauri ya Bahi walishafanya kampeni ya upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano hivyo, watoto wengi wanaoanza shule hivi sasa wanavyo vyeti hivyo na endapo ikitokea kuna mtoto hana cheti basi ataandikishwa shule ndipo mchakato wa kupata cheti hicho utafuata.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Charles Mduma amemueleza Waziri Jafo kuwa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza katika Wilaya ya Bahi ni 2,712.

Mduma alisema kuwa changamoto iliyokuwepo ni uhaba wa madawati ambayo tayari Halmashauri imeshaanza kuchonga madawati yatakayokidhi idadi ya wanafunzi hao.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mkakatika, John Laurent Josephat amesema shule yake ina lengo ya kaundikisha wanafunzi 180 na kwa siku ya kwanza tu baada ya shule kufunguliwa tarehe 06 Januari 2020, shule hiyo imeandikisha wanafunzi 134 sawa na asilimia 70.

“Wanafuzi wote walioletwa shuleni kwetu tumewaandikisha na endapo mtoto hana cheti cha kuzaliwa tulitumia Kadi ya Kliniki kupata taarifa sahihi za mtoto na hatujarudisha mwanafunzi hata mmoja wote wamepokelewa na wameanza masomo”. Alisema Mwl. Josephat.

 Shule ya Msingi Mkakatika, katika matokeo ya Darasa la Saba kwa mwaka 2019 ilishika nafasi ya kwanza kiwilaya na kimkoa ilishika nafasi ya tatu.


Picha na Matukio:

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ajili ya ziara ya siku moja kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika shule za sekondari tarehe 07 Januari 2020.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (kushoto) akitoa taarifa ya uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza katika shule za sekondari  kwa  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb) (kulia) tarehe 07 Januari 2020.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), akiwa katika Shule ya Sekondari Bahi ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku moja kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza shule za sekondari, tarehe 07 Januari 2020.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), (wa tatu kushoto), akipokelewa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mkakatika, John Laurent Josephat (wa pili kushoto) mara baada ya kuwasili shuleni hapo akiwa katika ziara ya kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza shule za sekondari, tarehe 07 Januari 2020.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), akiwa Shule ya Msingi  Mkakatika wilayani Bahi ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku moja kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza shule za sekondari, tarehe 07 Januari 2020.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), akiwa na wanafunzi wa Darasa la Kwanza wa Shule ya Msingi Mkakatika, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku moja kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza shule za sekondari, tarehe 07 Januari 2020.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (Mb), akiwa katika moja ya majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Bahi  ambapo baada ya ziara yake ya kukagua uandikishaji wa wanafunzi wa Darasa la Kwanza kwa shule za msingi pamoja na mapokezi ya wanafunzi wa Kidato cha Kwanza shule za sekondari, tarehe 07 Januari 2020, pia  alipita kukagua mandhari ya hospitali hiyo baada ya kukamilika.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa