• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mabati 780 Yanunuliwa, Mfuko wa Jimbo

Imechapishwa: February 12th, 2021

Na Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi.

Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo (Mb) amekabidhi mabati 130 kwa ajili ya kupaua vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu Shule ya Sekondari Bahi ambayo yanajengwa katikati ya vijiji vya Nagulo Bahi na Uhelela.

Nollo amekabidhi mabati hayo tarehe 12 Februari 2021 shuleni hapo ambayo ni miongoni mwa mabati 780 yenye thamani ya shilingi milioni 24.3 yaliyonunuliwa kwa fedha za Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuezeka madarasa 12 katika Shuke za Sekondari Mpinga (mabati 260), Ilindi (mabati 130), Mpamantwa (mabati 130), na Chibelela (mabati 130).

Akizungumza kabla ya kukabidhi mabati hayo, Nollo amewapongeza viongozi wa wilaya, Kata ya Bahi, Serikali za vijiji hivyo na wananchi kwa namna walivyojitoa katika michango ya fedha pamoja na kujitolea nguvu kazi kuhakikisha majengo hayo yanaenda kukamilika kwa wakati.

“Kwa jinsi nilivyolikuta jengo hili, na kwa jinsi mlivyoshirikiana viongozi na wananchi katika ujenzi huu  kupitia michango ya hali na mali, na mimi najiona bado nina deni jingine kwenu, hivyo pamoja na kutoa mabati haya leo bado kwa kutumia nguvu zangu na kwa kushirikiana na wadau mbalimbali nitajitahidi kuongeza majengo walau  mawili au matatu ili kuboresha shule hii.” Amesema Nollo.

Akizungumza katika makabidhiano ya Mabati hayo Diwani wa Kata ya Bahi, Augustino Ndonu amemshukuru Mbunge kwa kutoa mabati yote ya jengo hilo ambalo limejengwa kusaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika Shule ya Sekondari Bahi ambayo inahudumia vijiji vitatu vya kata hiyo yenye idadi kubwa ya wanafunzi wanaofaulu kujiunga na masomo ya Sekondari.

Aidha, Ndonu amemhakikishia Mbunge huyo pamoja na Serikali kuwa atahakikisha kila fedha ya serikali inayopelekwa katika kata yake ataisimamia vizuri na kuona inafanya kazi kama ilivyokusudiwa na siyo vinginevyo.

Awali, akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo Mkuu wa Shule ya Sekondari Bahi, Kudra Kitabuge amesema ujenzi huo ulianza tarehe 05 Januari 2021 kwa nguvu za wananchi pamoja na Serikali za vijiji mara baada ya kupokea agizo la kuanza kwa ujenzi huo kutoka ngazi ya wilaya.

“Hata hivyo, tarehe 08 Januari mwaka huu tulipokea kiasi cha shilingi milioni 12.5 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kwa ajili ya kusaidia ujenzi huu katika kuwalipa mafundi pamoja na vifaa mbalimbali hadi kufikia hatua hii ya upauaji, Mheshimiwa Mbunge tunakushukuru sana kwa kutupatia mabati haya ambayo yatasaidia kufunika jengo lote.” Amesema Kitabuge.

Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo (Mb) (aliyevaa suti ya kijivu) akikabidhi mabati 130 ya kuezekea vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu Shule ya Sekondari Bahi (Nagulo) tarehe 12 Februari 2021. Mabati hayo ni miongoni mwa mabati 780 yaliyonunuliwa na fedha za Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuezeka madara 12 ambayo ujenzi wake unaendele katika Shule za Sekondari Mpinga, Ilindi, Mpamantwa na Chibelela.

Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo (Mb) (aliyevaa suti ya kijivu) akizungumza kabla ya kukabidhi mabati 130 ya kuezekea vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu Shule ya Sekondari Bahi (Nagulo) tarehe 12 Februari 2021. Mabati hayo ni miongoni mwa mabati 780 yaliyonunuliwa na fedha za Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuezeka madara 12 ambayo ujenzi wake unaendele katika Shule za Sekondari Mpinga, Ilindi, Mpamantwa na Chibelela.

Baadhi ya viongozi wa Serikali za vijiji vya Bahi Sokoni, Nagulo Bahi na Uhelela wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kenneth Nollo (Mb) (hatupo pichani) kabla ya kukabidhi mabati 130 ya kuezekea vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu Shule ya Sekondari Bahi (Nagulo) tarehe 12 Februari 2021. Mabati hayo ni miongoni mwa mabati 780 yaliyonunuliwa na fedha za Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuezeka madara 12 ambayo ujenzi wake unaendele katika Shule za Sekondari Mpinga, Ilindi, Mpamantwa na Chibelela.

Muonekano wa jengo la vyumba viwili vya madarasa na ofisi moja ya walimu Shule ya Sekondari Bahi (Nagulo) ambalo ujenzi wake unaendelea litaezekwa kwa mabati 130 yaliyokabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Bahi, Kennth Nollo (Mb) (hayupo pichani) tarehe 12 Februari 2021. Mabati hayo ni miongoni mwa mabati 780 yaliyonunuliwa na fedha za Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuezeka madara 12 ambayo ujenzi wake unaendele katika Shule za Sekondari Mpinga, Ilindi, Mpamantwa na Chibelela. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa