• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Majaliwa Akemea Mikusanyiko ya Watoto Nyumba za Ibada

Imechapishwa: April 15th, 2020

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) amekemea mikusanyiko ya watoto (Madrasa na Sunday Schools) inayofanyika kwenye nyumba za ibada wakati akizungumza na viongozi wa mikoa kwa njia televisheni ifisini kwake Dodoma tarehe 15 Aprili 2020. Amesema kuwa imebainika kwamba baada ya masomo kusitishwa kwa sababu ya ugonjwa wa Covid 19 watoto wamekuwa wakienda kanisani na misikitini kwa ajili ya kujifunza.

"Naambiwa pamoja na kibali cha taasisi za dini kuendelea kumeanza mfumo wa kuanzisha madarasa ya watoto wadogo kwenye misikiti na makanisa inaitwa Sunday School inawakusanya vijana wengi, watoto wengi hilo pia ni sehemu ya maeneo ambayo tumeyawekea Kalantini hatutakuwa na Sunday School huo ni msongamano. Anasema Waziri Mkuu Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa amesisitiza kuwa alipokutana na Maaskofu na Mashekh walikubaliana kusitisha huduma nyingine zote isipokuwa Ibada tu. 

"Tumeruhusu Ibada tu... na ibada hiyo lazima iangaliwe iwe fupi inavyowezekana, tumezungumza vizuri na Mababa Askofu, tumezungumza pia vizuri na Mamufti wetu wa Tanzania Bara pamoja na wa Zanzibar kuhakikisha kwamba madrasa madrasa zinazoendeshwa humo, hizo Sunday Schools zote huwa hazipo, tulichoacha ni ibada". Anasema Waziri Mkuu Majaliwa.   

Amesema ni marufuku kwa watoto kukusanywa kwa kisingizio cha Sunday Schools au Madrasa. Amesema katika mazungumzo hayo kilichoachwa ni ibada ili ibada hizo zisaidie waumini kuliombea Taifa na amesema Serikali imesisitiza katika nyumba hizo za ibada waumini wake wajali kukaa kwa nafasi kama Wataalam wa Afya wanavyoshauri na tena ibada iwe kwa muda mfupi na baada ya ibada waumini watawanyike mara moja. 

Pia, Waziri Mkuu Majaliwa amesema makanisa ua misikiti haiwezi kuendesha makongamano ya kidini hivi sasa kwa sababu kongamano linahusisha watu wengi na wanatoka katika maeneo mbalimbali ambapo hiyo ni njia rahisi sana kupeleka maambukizi ya Covid 19. 

"Tusingependa sana tuingilie masuala ya dini lakini tunaamini Mababa Askofu, Mheshimiwa Mufti wa Bara na Zanzibar wanaelewa vizuri jambo hili na wao wataendela kutusaidia kuliratibu vizuri ili lisiweze kuleta madhara makubwa". Anasema Waziri Mkuu Majaliwa.   

Pamoja na katazo hilo, Waziri Mkuu Majaliwa aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali inatambua kuwa kuna masoko, maduka, Super Market na haikusudii kusitisha huduma hizo za kupata bidhaa kwenye maduka lakini muhimu zaidi, maduka yote yaweke ndoo za maji kwenye mlango na mteja anapoingia ndani awe ameshanawa ili anapochagua bidhaa ndani ya duka mikono yake iwe misafi na ikiwezeka hata anapotoka anawe. 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa