• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mganga: Bahi Lazima Mabadiliko Yatokee

Imechapishwa: February 6th, 2019

Benton Nollo, Bahi

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga amesema mabadiliko chanya katika Halmashauri hiyo ni lazima yatokee kwani anaamini uwezo wake wa kiutendaji kwa kushirikiana na watumishi waliopo wataipatia maendeleo wilaya hiyo na kuinua uchumi wa wananchi wa Bahi.

Mganga ameyasema hayo wakati akizungumza kwa lengo la kujitambulisha kwa watumishi wa Halmashauri hiyo waliopo Makao Makuu, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Bahi tarehe 06 Februari, 2019.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa anauhakika baada ya muda mfupi kwa kushirikiana wa Menejimenti na Wataalam mbalimbali waliopo Halmashauri hiyo itapiga hatua kimaendeleo na anaamini hicho ndiyo kitu pekee kitakachohalalisha uwepo wake Bahi.

“Ndugu watumishi kazi pekee iliyonifanya nije hapa ni kuleta mabadiliko, nikiwa hapa na pakaonekana hakuna mabadiliko kuja kwangu hapa ni kazi bure, ni lazima mabadiliko yatokeee hiyo jamani tupende tusipende ni lazima Bahi ya zamani ibadilike. Mimi sijawahi kuwa mahali popote mahali hapo pakawa pa mwisho. Hivyo, tushirikiane vizuri hasa katika suala la ukusanyaji wa mapato kwani mpaka sasa ni nusu mwaka lakini katika suala la ukusanyaji wa mapato Bahi imekusanya mapato kwa asilimia 24 na kiukweli hicho ndicho kipimo pekee ya kumpima Mkurugenzi katika nafasi yake”. Alisema Mganga.

Aidha, aliwataka watumishi kuamini kwamba uwepo wao katika Hamashauri ya Bahi ni neema na fursa ya pekee wao kuonesha kwamba wanaweza kufanya kitu chenye tija na faida kwa wananchi wa Wilaya ya Bahi.

“Binafsi mimi kuletwa Bahi ili nije kushirikiana na ninyi hiyo kwangu ni neema na fursa ambayo tunatakiwa kujua kuwa tunaweza kufanya kitu na tukaleta mabadiliko. Sasa yeyote atakayekuwa anakwaza hizo jitihada kwa kweli hatutahurumiana na wala sitakuonea aibu kwa sababu sisi wote tumeajiriwa na Serikali tuitumikie Serikali, tunapewa mishahara kwa sababu tunatakiwa tutumikie Serikali kwa hiyo mtu yeyote atakayekuwa anapokea mshahara lakini lengo lake halifikiwi huyo hapaswi kuwepo kwa sababu anaihujumu Serikali. Kwa hiyo kwa neno moja tu ninaomba tusaidiane kubadilisha hali ya Bahi. Alisema Mganga.

Kadhalika, Mganga aliwataka watumishi kutambua kuwa wanatakiwa kung’ara katika utendaji wao wa kazi na kusema kuwa hata Mungu hakumuumba mwanandamu kwa mtu wa chini bali alimuumba mwanadamu ili awe nuru katika uso wa dunia hii na kusisitiza kuwa watumishi wanapaswa kukerwa na malalamiko yanayotoka ngazi za juu kutoridhishwa na utendaji wa kazi wa Bahi na badala yake wafanye kazi kwa bidii na kwa kujituma.

Dkt. Fatuma Ramadhani Mganga ni Mkurugenzi mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi aliyeteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Januari, 2019 na kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 29 Januari, 2019.

.......................


Habari katika Picha:


Picha zote hapo juu ni Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi waliopo Makao Makuu wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Dkt. Fatuma Ramadhani Mganga (hayupo kwenye picha zote) wakati akijitambulisha kwa watumishi hao kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri tarehe 06 Februatri, 2019. (Picha zote na Benton Nollo)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa