• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Milioni 72 Mapato ya Ndani Zajenga Sekondari Nondwa

Imechapishwa: May 5th, 2020

Na Benton Nollo, Nondwa

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda ameipongeza Menejimenti na Halmashauri ya wilaya hiyo kwa kujenga madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu katika Shule ya Sekondari mpya ya Nondwa kwa shilingi milioni 72 ambazo ni mapato ya ndani.

Munkunda ameyasema hayo alipotembelea ujenzi huo tarehe 05 Mei 2020 akiwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo.

Pamoja na kuipongeza Halmashauri kwa kutoa fedha za mapato ya ndani shilingi milioni 55 kumalizia ujenzi wa majengo hayo, pia Munkunda  aliwapongeza wananchi wa Vijiji vya Nondwa na Zejele kwa mchango wa shilingi milioni 17 ambazo ni jitihada zao katika kuanzisha ujenzi huo.

“Viongozi wenzangu kama tunavyofahamu Kata ya Nondwa haina shule ya Sekondari hivyo, inawalazimu wanafunzi wa Nondwa na Zejele kutembea umbali wa takriban kilomita 20 kila siku kufuata masomo katika Shule ya Sekondari Chikopelo iliyopo Kata jirani ya Chali”. Anasema Munkunda.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga ameishukuru Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi kwa mchango wa mifuko 15 ya saruji aliyoitoa wakati wa ziara hiyo na kuisisitiza Kamati ya Ujenzi kuendelea na michango zaidi ili kukamilisha ujenzi wa choo ili shule ianze.

“Wenyeviti wa Vijiji wa Zejele na Nondwa wote mpo…jamani shime tumeshaona dalili kwamba shule yetu inaanza, tujenge vyoo lakini madarasa manne hayatoshi tujue kwamba hapa ndo tumeanza mchaka mchaka, shule kufikia Kidato cha Kwanza hadi cha Nne ni madarasa yasiyopungua hata kumi tufahamu hilo…na hivi sasa watoto wanafaulu kwa sababu elimu imeboreshwa sana”. Anasema Dkt. Mganga.    

Aidha, Wenyeviti wa Vijiji, Bernald Majuto (Nondwa) na Samsoni Mkwawi (Zejele) wameishukuru sana serikali kupitia Halmashauri hiyo kwa kuleta fedha hiyo ambayo imefanikisha ujenzi wa madarasa hayo pamoja na ofisi za walimu na wamewahakikishia viongozi hao kuwa ndani ya siku 30 vyoo vitakuwa vimekamilika.

Pia, viongozi hao wameahidi kwamba kwa kuwa jambo hilo limewafurahisha sana wananchi na wapo tayari kuchangia, hivyo kuanzia mwezi Juni 2020 Serikali za Vijiji zote mbili zimeshaweka mikakati ya kuanza michango ili kuanza ujenzi wa madarasa mengine mawili na ofisi ya walimu.

Muuonekano wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda akizungumza na viongozi wa Kata ya Nondwa (hawapo pichani) mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi  wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu kwa ajili ya shule mpya ya Sekondari Nondwa ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga akizungumza na viongozi wa Kata ya Nondwa (hawapo pichani) mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi  wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu kwa ajili ya shule mpya ya Sekondari Nondwa ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakikagua maendeleo ya ujenzi  wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu katika shule mpya ya Sekondari Nondwa ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.

Afisa Tarafa Chipanga, Christian Kiiza (kushoto) akiwashukuru wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Bahi kwa kukagua maendeleo ya ujenzi  wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu kwa ajili ya shule mpya ya Sekondari Nondwa ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nondwa, Bernald Majuto (kushoto) akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (hayupo pichani) aliyoifanya kukagua maendeleo ya ujenzi  wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu kwa ajili ya shule mpya ya Sekondari Nondwa ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Zejele, Samsoni Mkwawi akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (hayupo pichani) aliyekuwa akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi  wa madarasa manne (4) na ofisi mbili (2) za walimu kwa ajili ya shule mpya ya Sekondari Nondwa ambapo majengo hayo yapo katika hatua za umaliziaji.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MHE.KHADIJA SHABANI TAYA (KEISHA) ACHANGIA HUDUMA ZA AFYA KWA KUTOA MASHUKA 20 HOSPITALI YA WILAYA YA BAHI.

    May 12, 2025
  • MAFUNZO YA WAANDISHI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELETRONIKI YAFANYIKA JIMBO LA BAHI

    May 14, 2025
  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa