• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali Yakusanya Bilioni 2.9 Dodoma

Imechapishwa: May 3rd, 2021

Benton Nollo na Rosemary Celu (DMC), Bahi

Serikali ya Mkoa wa Dodoma imekusanya shilingi bilioni 2.9 kutoka katika sekta ya madini kwa mwaka wa fedha 2020/2021 ambapo asilimia 90 ya mapato hayo yanatokana na tozo mbalimbali za Serikali zinazolipwa na Wachimbaji Wadogo wa madini mkoani humo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwaWachimbaji Wadogo wa madini mkoani humo kuhusu namna bora ya uchukuaji wa sampuli za uchunguzi na uchenjuaji wa madini yaliyofanyika katika Mgodi wa Dhahabu wa Nholi uliopo wilayani Bahi tarehe 03 Mei 2021.

Dkt. Mahenge amefafanua kwamba, katika Sekta ya Madini Mkoa wa Dodoma kwa mwaka wa fedha 2020/2021 umepangiwa kukusanya shilingi bilioni 3 ambapo mpaka mwezi Aprili 2021 tayari mkoa huo umekusanya shilingi bilioni 2.9 sawa na asilimia 98 ya lengo.

“Utajiri huu tulionao tunataka uwafaidishwe wananchi wa Tanzania, na ndiyo maana marehemu Baba wa Taifa hakuyavuna kiholela holela, aliyachelewesha ili tuje tuyavune tukiwa na ujuzi wetu…leo kwa kuruhusu wachimbaji wadogo, maana yake kwa asilimia 100 wanaofaidika ni vijana wetu wa Tanzania…na ili mfadike ndiyo maana mafunzo haya leo yanatolewa”. Amesema Dkt. Mahenge.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema kwamba, kwa kuwa mafunzo hayo yatafanyika kwa nadharia na vitendo yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuleta matokeo chanya hali ambayo itasaidia kuinua uchumi wao na kuchangia mapato ya Serikali kutokana na tozo mbalimbali zinazotozwa katika sekta ya madini.

Akizungumza awali, Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi Munkunda, amesema kuwa awali Wachimbaji Wadogo katika Mgodi wa Dhahabu wa Nholi walikuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya umeme, maji nabarabara ya kufika mgodini hapo, ambapo kwa sasa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeboresha miundombinu hiyo.

“Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, Wilaya ya Bahi pamoja na mambo mengine kwa sasa ndiyo wazalishaji wakubwa wa madini ya dhahabu, …na hawa unaowaona hapa mbele yako ndiyo wazalishaji wenyewe na ndiyo maana kila wanachokiomba kwetu kama Serikali tunakileta mara moja”. Amesema Munkunda na kuongeza;

“Tunakileta kwa haraka kwa sababu tunafahamu wawekezaji hawa hatutakiwi kuwachelewesha na tunawapa thamani kama walivyo wawekezaji wengine wakubwa, hawa ni wawekezaji wetu wa ndani, ndani ya wilaya, kwahiyo tunawapa thamani ile ile kama walivyo wawekezaji wengine wakija wa nje.”

Munkunda ameishukuru Wizara ya Madini kuputia Tume ya Madini kwa kuendesha mafunzo hayo ambayo amesema yatakuwa msaada mkubwa kwa Wachimbaji Wadogo na yatasaidia kuokoa uharibifu mkubwa wa mazingira katika eneo la machimbo.

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Nchangwa Marwa, amesema lengo la kuandaa mafunzo hayo ni kuongeza ujuzi wa uchimbaji wa madini pamoja na kujua namna ya uchukuaji wa sampuli na uchenjuaji kwa wachimbaji wa madini ili kuboresha mazingira kwa wachimbaji wadogo. 

“Suala la utafiti kwenye uchimbaji mdogo, kukosa ujuzi wa utambuzi wa miamba, pamoja na namna ya uchukuaji wa sampuli kupeleka maabara, hata kutafsiri majibu ya maabara, imekuwa ni shida kubwa kwa wachimbaji wadogo. Hali ambayo ilisababisha uchimbaji wao uwe ni wa kubahatisha…Serikali ya Wamu ya Sita imekusudia kuboresha mazingira ya uchimbaji”. Amesema Mhandisi Marwa.

Mhandisi Marwa amesema ili kupata ufanisi na tija, ofisi yake imekubaliana na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) kutoa mafunzo kwa kundi moja moja na mafunzo hayo kwa kuanzia, yanaanza na Wachimbaji wa Madini ya Dhahabu na baadae kumaliza makundi mengine ya uchimbaji.

Naye, Diwani wa Kata ya Mpalanga, Baraka Ndhahani ameishukuru Serikali kwa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Wachimbaji Wadogo katika Mgodi wa Dhahabu wa Nholi hasa ujenzi wa barabara na umeme.

Ndahani amesema pamoja na maboresho hayo uongozi katika mgodi huo umejipanga kuanza ujenzi wa Kituo cha Polisi, Zahanati na Shule Shikizi ambapo tayari tripu 10 za mchanga zimeshasombwa na michango inaendelea. Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma papo hapo baada ya kupewa taarifa hiyo naye kupitia ofisi yake alichangia mifuko 100 ya saruji ambayo alielekeza itumike kujenga Kituo cha Polisi mgodini hapo.

 Akishukuru kwa niaba ya Wachimbaji Wadogo, Meneja wa Mgodi wa Dhahabu wa Nholi, Kulwa Limbu, amesema kitendo cha Serikali kupeleka huduma ya nishati ya umeme na kuchonga barabara kutoka Kijiji cha Mzogole kuingia mgodini hapo kumeleta faraja na imani kubwa kwa serikali yao kwamba inawajali, inawatambua na inathamini mchango wao katika kuchangia kukuza uchumi wa nchi yao.


Matukio katika Picha:

(Picha zote na Benton Nollo)

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa