• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wanawake Dodoma Wamshukuru Rais Dkt. Magufuli

Imechapishwa: March 8th, 2021

Benton Nollo na Bernard Magawa (DMC), Bahi.

Wanawake Mkoani Dodoma wamempongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwamba kupitia Serikali ya Awamu ya Tano amewapa kipaumbele akina mama wengi kwa kuwateua  katika nafasi mbalimbali za uongozi hali ambayo imewawezesha kushiriki ngazi mbalimbali za maamuzi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda tarehe 8 Machi, 2021 ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya kilele cha Siku ya Wanawake Duniani ambapo kwa Mkoa wa Dodoma yamefanyika kimkoa wilayani Bahi.

“Tunampongeza sana Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ametuheshimisha sana Wanawake wa Tanzania kwa kutupa kipaumbele  katika nafasi mbalimbali za uteuzi akiwemo Makamu wa Rais wa Nchi yetu Mama Samia Suluhu Hassan ambaye anachapa kazi kwa bidii na hajawahi kutuangusha wanawake wenzake.” Amesema Munkunda.

Akizungumza kwenye maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa machi 8 kila mwaka kwa lengo la kuhamasisha usawa kati ya Wanaume na Wanawake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Queen Mlozi amewataka wanawake waliopewa madaraka mbalimbali kuhakikisha wanawashika mkono wanawake wengine ili kwa pamoja washikamane  katika kutetea haki za wanawake wenzao.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Josephat Maganga akizungumza kwa niaba ya Wanaume waliohudhuria maadhimisho hayo yenye kauli mbiu isemayo ‘Wanawake katika uongozi chachu ya kufikia Dunia ya usawa’, amewapongeza wanawake wote walio na nafasi mbalimbali za uongozi kwa jitihada za dhati katika nafasi walizopewa na kuwaasa wanawake wote nchini kusimamia kikamilifu malezi ya watoto wa kike ili kuwaandaa kuwa viongozi wa baadaye.

 Awali akiwakaribisha Wageni mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo katika uwanja vya Singidani Bahi mjini, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma Mganga amesema wilaya yake imekuwa ya mfano mkoa wa Dodoma katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya serikali hasa utekelezaji wa miradi kwa ufanisi na kumuonyesha matumaini Rais wa Tanzania kwamba hakukosea kuwateua na kwamba wanawake ni waaminifu sana na wakipewa nafasi katika Uongozi wanawajibika ipasavyo.

Picha na Matukio:

Maandamano yakipita mbele ya Mgeni Rasmi 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi akiwasalimia Wanawake na wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021.

Waheshimiwa Madiwani Wanawake wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021.

Katibu Mkuu Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Queen Mlozi (aliyevaa kilemba cha bluu) akimkabidhi Kiti Mwendo (wheel chair) Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Phillipina Philipo (kulia) kilichotolewa na na Karakana ya Walemavu Dodoma (KAWADO) ili itumike katika Hospitali ya Wilaya ya Bahi  wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021. Pamoja na kiti hicho pia, KAWADO wametoa kiti kingine kimoja kwa Mwanafunzi Mwenye Ulemavu, Brian Msendekwa wa Shule ya Msingi Mphangwe na Baiskeli moja ya magurudumu matatu kwa Mwanafunzi Mwenye Ulemavu, Vaileti Maloda wa Shule ya Msingi Lamaiti. Anayeshuhudia katikati ni Mgeni Rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi Munkunda.

Picha za juu ni Katibu Mkuu Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Queen Mlozi (kushoto) pamoja na viongozi mbalimbali wakikabidhi msaada wa nguo zilizokusanywa na Tasisi ya Vijana ya Active Hope kutoka kwa watu mbalimbali wenye uwezo kwa ajili ya kuwapatia wahitaji,  wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021.

Wananchi mbalimbali wamejitokeza kuchangia damu ili kuwasaidia akina mama na watoto wenye uhitaji, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021.

Baadhi ya akina mama wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021.

Walimu Wanawake wa Shule ya Msingi Bahi Misheni na Shule ya Sekondari Bahi wakiimba shairi maalum wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba (kulia) akiteta jambo na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Pius Mwaluko (kushoto) wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo yamefanyika wilayani Bahi kimkoa tarehe 08 Machi 2021. (Picha zote na Benton Nollo).


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa