• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Watendaji Kata, Vijiji Wapongezwa Bahi

Imechapishwa: July 15th, 2019

Benton Nollo na Alinikyisa Humbo

Watendaji wa Kata na Vijiji wilayani Bahi wamepongezwa kwa kusimamia vema ukusanyaji wa mapato baada ya kuvuka malengo ya makusanyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Dkt. Fatuma R. Mganga  kwa Watendaji wa Kata 20 kati ya Kata 22 na Watendaji wa Vijiji 45 kati ya vijiji 59 wilayani humo kwa kukusanya mapato ya vibali vya mifugo kwa zaidi ya asilimia 80 ya malengo waliyokuwa wamewekewa kwa mwaka huo.

Dkt. Mganga ameyasema hayo  Julai 15, 2019 katika kikao kazi alichokiitisha cha Watendaji wa Kata na Watendaji wa Vijiji kwa lengo la kufanya tathmini ya ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2018/2019 na kupeana malengo mapya kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

Akizungumza na Watendaji hao, Dkt. Mganga amesema kuwa anawapongeza sana Watendaji wote waliofikia lengo na wengine kuvuka lengo katika suala zima la ukusanyaji wa mapato hasa ya vibali vya mifugo.

Dkt. Mganga amesema Watendaji wote waliofanya vizuri kwa kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato katika maeneo yao watatunukiwa vyeti maalum vya kutambua juhudi zao katika ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri ikiwa ni pamoja na kuwapatia vitendea kazi ili kurahisisha zaidi ukusanyaji wa mapato kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

 “Kata zote zilizofanya vizuri na zilizovuka malengo ya makusanyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Watendaji husika watapatiwa motisha na Halmashauri pamoja na vyeti maalum ikiwa ni kutambua mchango wao katika kukusanya mapato ya serikali na kwa wale waliofanya vibaya nao watapatiwa stahili yao”. Alisema Dkt. Mganga.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa malengo ya makusanyo ya mapato ya vibali vya mifugo kwa kila kata na kijiji, Kaimu Mweka Hazina wa wilaya hiyo Arbogast Chrisant alizitaja kata 20 zilizofanya vizuri ,ambazo ni  Chikola,Chipanga, Msisi, Ibihwa, Ilindi, Nondwa, Mtitaa, Bahi, Kigwe  na Lamaiti. Kata nyingine Chali,Makanda, Mpalanga, Mundemu, Chifutuka, Chibelela, Mwitikira, Mpinga, Zanka na Babayu. Hata hivyo, Chrisant alisema kata 2 za Mpamantwa na Ibugule hazikufikisha malengo.

Aidha, kwa upande wa vijiji vilivyofanya vizuri Chrisant alivitaja kuwa ni Chikola ,Tinai, Magaga, Chipanga “B”, Nkulughano,  Chimendeli,  Nchinila,  Mnkola,  Msisi,  Nagulo Bahi,  Chiguluka, Chipanga “A” na Bahi Makulu. Vijiji vingine ni Mindola,  Chidilo,  Chali Igongo,  Zejele,  Mundemu,   Nondwa,  Ilindi,  Chali Makulu,  Kisima cha Ndege,  Chikopelo ,  Lamaiti,  Kigwe,  Zanka, Bankolo, Chonde, Mpalanga, Bahi Sokon,.Msisi,  Chibelela,  Kigwe, Makanda,  Mpinga,  Mtitaa,  Babayu, Lamait,  Bahi,   Mwitikira, na M Mundemu,  hata hivyo Chrisant  alivitaja vijiji ambavyo havikukusanya mapato kufikia asilimia 50% kuwa ni vijiji 14 ambavyo ni Ikumbulu, Chibelela, Mayamaya , c Chifutuka, Nkhome, Asanje, Mzogole, m Mpamantwa,  Mkondai,  Mapanga,  Chali  Isanga, Ibugule,  Nholi, na kijiji cha Mkakatika.

Akijibu taarifa hiyo Dkt  Mganga  ameseama kuwa Kata na Vijiji vilivyofanya vizuri vitapewa zawadi ya vyeti na pia aliwataka Watendaji wa Vijiji na Kata ambazo hazikuweza kufikia lengo kuendelea kutafuta mbinu mbadala ya kuweza kukusnya mapato hiyo ili kuweza kutimiza lengo la Serikali katika ukusanyaji wa mapato mbalimbali ya Serikali .

Dkt  Mganga amesema kuwa miongoni mwa Kata zilizofanya vizuri Kata tatu bora zitapewa zawadi lakini pia alisistiza kuwa Kata mbili ambazo hazikufanya vizuri zitawajibishwa

Mbali na taarifa ya mapato Dkt  Mganga alizungumzia suala la uadilifu na nidhamu katika kazi alisema kuwa kiongozi yeyote anayejitambua hata utendaji wake wa kazi unakuwa bora na wenye uadilifu wa hali ya juu lakini pia alitoa rai kwa Watendaji wa Kata na Vijiji kuwa waadilifu katika majukumu waliopewa ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika kufanya na kutimiza wajibu wa Serikali

“Hii Halmashauri ni yetu sote basi tukipewa majukumu tufanye kwa uadilifu na tutimize malengo na majukumu mbalimbali ambayo tumepewa na Serikali pia tuheshimiane na kufuta taratibu zote za kikazi hakuna kinachoshindikana vyote vinawezekana tukizingatia uadilifu katika kazi”alisema Dkt  Mganga.

Na katika kuendelea kusisistiza suala la uadilifu kazini Kaimu Afisa utumishi, Chrispine Katalyeba  amewataka watendaji kuacha kufanya kazi kwa mazoea na kwamaba kila mmoja afuate utaratibu uliopokulingana sheria ya kazi,pia aliwataka kuzingatia sheria ya mavazi katika utumishi wa umma,laini pia aliwaasa kuepuka kupokea au kutoa rushwa kwani nikosa kisheria.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa