• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Waziri Ummy: Serikali Haijapiga Marufuku Zebaki

Imechapishwa: March 5th, 2021

Benton Nollo 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu amesema Serikali haijapiga marufuku uingizaji na utumiaji wa kemikali aina ya Zebaki na badala yake imewataka waingizaji na wasambazaji kujisajili kwenye maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali.

Ummy ameyasema hayo wakati akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika Kijiji cha Nholi wilayani Bahi tarehe 05 Machi 2021 alipofanya ziara ya kikazi kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo.

Waziri Ummy amesema kuwa asilimia 80 ya kila kilo 100 za zebaki zinazoingizwa nchini hutumika katika shughuli za uchenjuaji hivyo, Serikali inawajibika kupunguza matumizi ya kemikali hiyo ifikapo 2025.

“Ndugu zangu napenda kusisitiza zebaki si haramu na si madawa ya kulevya na wala si bangi hivyo wanaoingiza au kusambaza msijifiche, hamtakamatwa. Sisi Ofisi ya Makamu wa Rais na Wizara ya Madini tutashirikiana kwa pamoja kuhakikisha tunapata teknolojia mbadala na rahisi ya kuchenjua dhahabu isiyo na madhara kwa binadamu.” Amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri huyo amesema ripoti ya Shirika la Afya Duniani – WHO imebainisha kwamba zebaki ni moja ya kemikali hatari zaidi na kuwa inahatarisha afya ya binadamu kwani inaweza kusababisha magonjwa ya saratani na figo pamoja na madhara kwa wanyama na mimea.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amewataka wachimbaji hao kutunza mazingira yanayowazunguka mgodini hapo kwa kutokata miti ovyo ili kutumia katika shughuli za uchimaji wa madini badala yake wapate vibali vya kuitumia miti hiyo.

Pia, amewataka wachimbaji hao wasiache masimo wazi wakati wanapotafuta maeneo yenye dhahabu na badala yake wayafukie pamoja na na kuhakikisha zebaki haisambai ovyo kwa inaweza kuleta madhara.

Ummy amesema Serikali inawatambua wachimbaji wadogo kwa kuwa wanajipatia kipato kutokana na shughuli hiyo na pia kupitia wao Serikali inapata mapato.

Kadhalika, Waziri Ummy amesisitiza na kuwataka wamiliki wa migodi kuwapatia vifaa kinga (Protective Gears) wafanyakazi wao ili kuwaepusha na madhara ya zebaki na kuahidi kujengwa kwa kituo cha umahiri cha uchimbaji ili wachimbaji wa eneo hilo wajifunze.   

Awali, akizungumza Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mwanahamisi  Munkunda amesema Serikali ya Wilaya hiyo imesogeza huduma muhimu katika eneo hilo hasa umeme ambao umesaidia kurahisisha utendaji kazi kwani mashine mbalimbali mgodini hapo sasa zinatumia umeme na amemuaomba Waziri Ummy kwamba Kituo cha Umahiri cha Madini kijengwe wilayani Bahi kwa kuwa ndiyo wilaya inayoongoza kwa uzalishaji wa madini mbalimbali mkoani Dodoma.

Naye, Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Nchagwa Marwa amesema katika kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2020 hadi Februari 2021 Mgodi wa Nholi umezalisha zaidi ya kilo 47.24 za madini ya dhahabu ambazo zimeuzwa kwa zaidi ya shilingi bilioni 5 na kuipatia Serikali mrabaha wa shilingi milioni 300 huku Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ikipata shilingi milioni 17 kama gawio kwa mujibu wa Sheria za Madini hapa nchini.

 Awali akitoa taarifa ya shughuli za uchimbaji wa madini mgodini hapo, Meneja wa Mgodi huo, Kulwa Limbu amesema mgodi huo una leseni 100 ambapo kati ya hizo leseni 4 tu zipo hai, mashimo au maduara 100 yenye zaidi ya wachimbaji 500 na kuongeza kuwa changamoto kubwa katika eneo hilo ni kukosekana kwa maji safi na salama kwa matumizi ya wachimbaji hao pamoja na ubovu wa barabara ya kutoka Dodoma mjini kulifikia eneo hilo.

Matukio katika Picha:

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu (kulia) akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika Kijiji cha Nholi wilayani Bahi  alipofanya ziara ya kikazi kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo tarehe 05 Machi 2021.

Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda (kulia) akizungumza na wachimbaji wadogo wa dhahabu katika Kijiji cha Nholi wilayani Bahi wakati wa ziara ya kikazi iliyofanywa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira (hayupo pichani) kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo tarehe 05 Machi 2021.

Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Nchagwa Marwa (katikati) akifafanua jambo mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira (wa kwanza kushoto) wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira Mgodi wa Dhahabu wa Nholi tarehe 05 Machi 2021. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda.

Meneja Mgodi wa Dhahabu Nholi, Kulwa Limbu akiwasilisha changamoto wachimbaji wadogo mgodini hapo wakati wa ziara ya kikazi iliyofanywa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira (hayupo pichani) kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo tarehe 05 Machi 2021.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wa dhahabu katika Kijiji cha Nholi wilayani Bahi wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu alipofanya ziara ya kikazi kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo tarehe 05 Machi 2021.

Picha zote juu ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu (mwenye mtandio wa bluu) alipotembelea Mgodi wa Dhahabu Kijiji cha Nholi wilayani Bahi  wakati wa ziara ya kikazi kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo tarehe 05 Machi 2021.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu (mwenye mtandio wa bluu) alipotembelea Mgodi wa Dhahabu Kijiji cha Nholi wilayani Bahi  wakati wa ziara ya kikazi kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira mgodini hapo tarehe 05 Machi 2021. Picha za juu ni Waziri Ummy akikagua Mgodi Mdogo wa kuchenjua dhahabu kwa kutumia Cyanide (CIL) unaomilikiwa na Kampuni ya Binslum. 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa