• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Changamoto za Bahi Zamsononesha Waziri Mabula

Imechapishwa: January 23rd, 2019

Benton Nollo, Bahi

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula (Mb) amekutana na changamoto nyingi zinazoikabili Halmashauri ya Wilaya ya Bahi hali iliyomsononesha na kushindwa kuwabana Wataalam wa Idara ya Ardhi na Maliasili Wilayani humo.

Akiwa katika ziara ya kikazi ya siku moja wilayani humo kuhamasisha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kupitia sekta ya ardhi tarehe 23 Januari 2019, Mabula aliikuta Halmashauriya Wilaya ya Bahi ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu wa bajeti pamoja na uhaba wa vitendea kazi hasa magari.

Hali ambayo imesababisha Halmashauri kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kama vile suala la ukusanyaji wa mapato ya Serikali yanayotokana na sekta ya ardhi, kuwapelekea hati za madai wadaiwa sugu wa kodi za ardhi, kupima na kupanga viwanja pamoja na kwenda kuwaelimisha wananchi kuhusu matumizi bora ya ardhi.

“Sekta ya ardhi ni Idara nyeti sana ambayo inaweza kuiingizia Serikali Mapato mengi lakini kama haitawezeshwa kufanya kazi ipasavyo kwa kupatiwa rasilimali fedha na vifaa kama magari basi itashindwa kutekeleza majukumu yake na hivyo kuifanya Serikali kukosa mapato kupitia sekta hiyo”. Alisema Mabula.

Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Chedieli Mrutu alimueleza Naibu Waziri Mabula kuwa, Idara yake haijawahi kupatiwa fedha zinazotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri na kutaja kuwa bajeti ya Idara hiyo kwa mwaka ni shilingi milioni 2.5 na kubainisha kuwa wakati mwingine fedha hiyo haipatikani kabisa.

Mrutu alimueleza Naibu Waziri Mabula kuwa Idara hiyo haina gari kabisa ambalo kimsingi lingeiwezesha Idara yake kufanya kazi za ardhi ambazo wakati mwingine wataalamu wanantakiwa kwenda umbali mrefu kuwahudumia wananchi katika masuala ya ardhi.

Kufuatia hali hiyo, Mabula alitaka kufahamu mgao wa fedha za mapato ya ndani kwa Halmashauri hiyo kwa idara na vitengo vyote vya Halmashauri kwani kwa uzoefu katika maeneo mengi aliyopita nchini alisema Idara ya ardhi imekuwa mtoto yatima kwani inatengwa na kupatiwa kiasi kidogo cha fedha ukilinganisha na idara nyingine hali ambayo kwa Halmashauri ya Bahi baada ya kuhoji hakuna tofauti jambo lililomfanya aishiwe nguvu na kusema kuwa kiukweli Halmashauri ya Bahi inahitaji kusaidiwa na kuangaliwa kwa jicho la pekee.

Mabula alisema kiasi cha shilingi milioni mbili na laki tano kilichotengwa kwa ajili ya Idara ya Ardhi na Maliasili kwa mwaka hakiwezi kufanya kitu kwani idara hiyo ina majukumu mengi sana na hali hiyo ndiyo iliyosababisha makusanyo yawe kidogo kwani mpaka Desemba 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi ilikuwa imekusanya shilingi milioni saba ilhali malengo iliyowekewa ni kukusanya shilingi milioni 47.

Aliongeza kuwa kwa hali ilivyo Halmashauri ya Wilaya ya Bahi haiwezi kufikia asilimia hamsini ya malengo ya Serikali. Hivyo, aliiagiza Ofisi ya Kamishna Msaidizi Kanda ya Kati kuona namna ya kuisaidia Idara hiyo angalau iweze kutatua baadhi ya changamoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Leo Mavika alisema Halmashauri yake inakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa fedha kwani mapato ni kidogo. Aidha, alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto hiyo Halmashauri itajitahidi kuhakikisha kuwa kiasi kidogo cha mapato kitakachopatikana kitagawanywa sawa katika Idara na Vitengo vyote huku Idara ya Ardhi na Maliasili ikipewa kipaumbele kutokana na umuhimu wake.

Aidha, Mavika alimuomba Naibu Waziri huyo kama inawezekana kuisaidia Idara hiyo gari kwani kwa sasa Halmashauri ina magari mazima mawili tu jambo ambalo linafanya utendaji wa shughuli za Halmashauri za kila siku kuwa mgumu sana.  

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Munkunda alisema kuwa ili WIlaya yake itoke mahali ilipo inahitaji mikakati madhubuti na msukumo wa kipekee hasa wa vitendea kazi kwani hali hiyo ndiyo inayowakatisha tamaa watumishi kutokana na kushindwwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kuwepo changamoto hizo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa