• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
BAHI DISTRICT COUNCIL
BAHI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kazi na Moto
      • Afya
      • Maji
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Ardhi na Maliasili
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Teknolojia na Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Baraza la Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mpiango
      • Ujenzi,Uchumi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili ya Madiwani
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokubaliwa
    • Miradi Inayoendelea
      • TASAF
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Kazi
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbali Mbali
    • Miongozo Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video Mbali Mbali
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MaMEK, Walimu Wakuu waagizwa kusimamia walimu

Imechapishwa: March 27th, 2018

Na Benton Nollo,

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Bahi, Daniel Kehogo amewataka Waratibu Elimu Kata (MEK) na Walimu Wakuu wote Wilayani humo, kuhakikisha kuwa wanawasimamia vema walimu hususan ufundishaji shuleni kwa kuwatembelea mara kwa mara ikiwa ni pamoja na kujua maendeleo ya wanafunzi ili kuinua kiwango cha ufaulu katika mtihani wa Darasa la Saba wa mwaka 2018.

Kehogo aliyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa Waratibu Elimu Kata 22 na Walimu Wakuu 72 kuhusu ujazaji wa madodoso ya Takwimu za Shule za Awali (TSA), Takwimu za Shule za Msingi (TSM) na Takwimu za Elimu ya Watu Wazima (TWM), yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Bahi tarehe 27 Machi 2018.

“Ndugu zangu tukumbuke kuwa katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba ya mwaka 2017, Halmashauri yetu ilishika nafasi ya tano katika mkoa wa Dodoma. Hivyo, sisi kama viongozi tutambue kuwa tunao wajibu mkubwa sana kuhakikisha kuwa wanafunzi wanafundishwa na kuelewa ipasavyo masomo yao wawapo darasani ili katika mtihani wa Darasa la Saba wa mwaka 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi iwe ya kwanza kimkoa na kitaifa”. Alisema Kehogo.

Kehogo aliwaeleza washiriki kuwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kupitia Halmashauri, inalo jukumu la kukusanya takwimu za Elimu ya Awali, Msing, Sekondari, Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi ambazo hukusanywa kila mwaka mwezi Machi kwa kutumia Dodoso la Shule au Kituo kinachotoa elimu kwa ngazi husika.

 “Takwimu hizi hutumikakutoa taarifa na picha ya hali halisi iliyofikiwa kutokana na viashiria mbalimbali vya kielimu katika Sekta ya Elimu Msingi na Elimu ya Sekondari Kidato cha Tano na Sita ambavyo huonesha ni kwa kiasi gani utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo imefanikiwa”. Alifafanua Kehogo na kuongeza;

“Ili kufikia lengo hilo la ukusanyaji wa taarifa hizo muhimu kwa usahihi, mafunzo haya yameandaliwa ili kuwawezesha wanaohusika kuelewa kwa ufasaha maswali na takwimu zinazohitajika ili kufanikisha zoezi lengwa na ni muhimu kusoma maelekezo kwa makini kabla ya kuanza ujazaji wa Dodoso”.

Awali akimkaribisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya, Afisa Elimu Msingi, Mohammed Msongo, amewasihi Waratibu Elimu Kata na Walimu Wakuu kufanya kazi kwa ushirikiano na walimu kwani wao kama viongozi wanawajibu wa kutambua na kutatua changamoto zinazowakabili walimu hata kabla ya walimu wanaowaongoza kuwapelekea.

“Tafadhali ndugu zangu tatueni changamoto za walimu katika maeneo yenu. Kiongozi mzuri na mahiri ni yule mwenye uwezo wa kujua changamoto za wale anaowaongoza hata kabla ya wahusika kumueleza”. Alisema Msongo na kuongeza;

“Hakikisheni ninyi kama viongozi mnachapa kazi ili kuleta tija katika sekta ya elimu na ikumbukwe kuwa kipimo kwamba tunafanya kazi ni pale yanapotoka matokeo ya wanafunzi katika mitihani ya Taifa”.

Usahihi wa takwimu za Elimu Msingi ni miongoni mwa vipengele vinavyopimwa katika utoaji wa fedha za Ruzuku ya “Elimu Lipa kwa Matokeo – EP4R” ambazo hutolewa kila mwaka na Serikali kwa lengo la kuboresha miundombinu ya shule, ikama ya walimu, ufuatiliaji wa taaluma shuleni pamoja na uboreshaji wa Mfumo wa Ukusanyaji wa Takwimu za Elimu Msingi (BEMIS) ambapo kupitia Mpango wa EP4R Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ilipatiwa shilingi 187,287,311.00.

 Fedha hizo zilipangwa kutekeleza shughuli zifuatazo; Ufuatiliaji, Takwimu, Usimamizi na Tathmini shilingi 18,728,628.00 sawa na 10%, Ikama ya Walimu (Elimu Msingi) shilingi 37,457,257.46 sawa na 20%, Ujenzi wa Madarasa shilingi 74,914,514.92 sawa na 40% na Umaliziaji Maabara shilingi 56,185,886.19 sawa na 30%.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO May 07, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI May 02, 2025
  • Mikopo ya Hazina Kwa Watumishi wa Umma October 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU (Limetolewa kwa kuzingatia kanuni ya 8(1) February 20, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC JOACHIM NYINGO AKABIDHI VIFAA VYA SHULE VYA MILIONI 5.3

    May 06, 2025
  • MWENGE WAZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI MOJA MILIONI MIA TANO KUMI NA SABA LAKI NANE ELFU MIASITA THEMANINI NA NANE NUKTA SITA.(TSH.1,517,414,684.63) KATIKA WILAYA YA BAHI.

    April 25, 2025
  • MKOA WA DODOMA WAPOKEA RASMI MWENGE WA UHURU 2025.

    April 20, 2025
  • KARUME DAY

    April 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Jinsi ya kuomba uhamisho kwenye mfumo wa Utumishi
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Tazama na Kudownload Orodha ya Walioitwa Kwenye Interview kwa Nafasi za Watendaji wa Vijiji Bahi
  • Matokeo Kidato cha Nne 2017
  • Tazama matokeo ya Darasa la saba 2019 ya shule zote za Bahi
  • Tazama na Kudownload vigezo vya Nafasi za Kazi kwa Watendaji wa Vijiji
  • Matokeo ya QT
  • 1: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Darasa la Nne (SFNA) 2017
  • Vendor Form
  • 2: Matokeo ya Upimaji wa Kitaifa Kidato cha Pili (FTNA) 2017

Viunganishi Linganifu

  • NECTA
  • Mfumo wa uhamisho kwa watumishi,Mikopo na Kupata Salary Slips
  • Utumishi
  • OR-TAMISEMI
  • Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  • Tovuti ya Mkoa wa Dodoma

Watembeleaji wa Nje

world map hits counter

Watembeleaji

Counter Widgets

Ramani

Wasiliana Nasi

    Kitengo cha Ugavi na Manunuzi

    Anuani: S.L.P 2993 DODOMA

    Simu: +255 762077589

    Simu: +255 762077589

    Barua Pepe: ded@bahidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Bahi. Haki Zote Zimehifadhiwa